Na Mwandishi Wetu – Pawaga Iringa.
Mhandisi
wa Umwagiliaji Mkoa wa Iringa ONESMO KAHOGGO amewataka viongozi katika
Skimu za Umwagiliaji kusimamia kikamilifu zoezi la ukusanyaji ada na
tozo kwa lengo la kutunisha mfuko wa Umwagiliaji.
Akizungumza
mjini IRINGA Bw, KAHOGGO amesema endapo wakulima katika Skimu za
Umwagiliaji watachangia fedha za ada ya usajili na matunzo kwa wakati,
itasaidia kuharakisha ukarabati wa Skimu zilizoharibika kutokana na
athari zitokanazo na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi pamoja na
kujenga Skimu mpya nchini.
Ametolea
mfano zoezi la kuurejesha mto Ruaha Mdogo katika njia yake ya asili
limegharimu fedha kutoka mfuko wa Umwagiliaji ambao unahitaji kuwezeshwa
na wakulima hao.
Kwaupande
wake Bi, KATARINA RASHIDI MLAGA mkulima mkazi wa kijiji cha Magozi
ameishukuru serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa kazi kubwa
iliyofanya wa kurejesha mto Ruaha Mdogo katika njia yake ya asili,
nakusema kuwa wakulima katika kijiji hicho hutegemea Zaidi kilimo cha
umwagiliaji, na wamepata elimu ya kutosha kuhusu uchangiaji wa tozo za
umwagiliaji na wapo tayari kuchangia.
Awali
akiongea kijijini hapo Diwani wa kata ya ILOLO MPYA Bw, FUNDA MIHAYO
amemshukuru Mkurugenzi wa Tume ya taifa ya Umwagiliaji Bw, DAUDI KAALI
kwa kuwezesha wataalam wa tume kurekebisha miundombinu ya mifereji ya
kupeleka maji katika mashamba ya wakulima pamoja na zoezi la usanifu
linaloendelea katika Skimu ya Liganga ambapo lengo ni kuwezesha maji
kunyweshea Skimu ya Magozi na Mkombilenga.
Mhandisi
Umwagiliaji Mkoa wa Iringa Bw. Onesmo Kahoggo akingumza kuhusu Viongozi
wa skimu za kilimo cha Umwagiliaji Nchini, kusimamia ukusanyaji wa ada
na Tozo za Umwagiliaji.
Bi
Katarina Rashid Mlaga, mkulima mkazi wa kijiji cha Mgozi akiishuru
Serikali kwa kurejesha mto Ruaha Mdogo katika njia yake ya asili.
Picha Ikionesha mto Ruaha mdogo baada ya kurejeshwa katika njia yake ya asili.
Picha ikionesha Roli la kubebea mchanga likiwa kazini wakati wa ukarabati wa mto Ruaha mdogo.
No comments:
Post a Comment