Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imetoa elimu kwa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi kuhusu matumizi sahihi ya ardhi kwenye maeneo yanayozunguka viwanja vya ndege nchini.
Elimu
hiyo imetolewa na Mkaguzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege Tanzania Mhandisi.
Bernard Kavishe kwa kupitia mada aliyoiwasilisha katika mkutano mkuu wa
pili wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji
Majenzi (AQRB)uliofanyika tarehe 07 mpaka 08 Oktoba, 2021 junguliwa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa jijini Arusha.
Hafla hiyo ya ufunguzi ilihudhuriwa na viongozi
wa serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella, Mkuu wa
Wilaya ya Arusha Mhe. Sofia Mjema na Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe.Frank
Mwaisumbe.
“Sote
ni mashahidi kuwa miaka ya hivi karibuni serikali imeamua kuwekeza
fedha nyingi katika ujenzi wa viwanja vya ndege na ununuzi wa ndege
hivyo ni vyema sote tukawa na uelewa wa pamoja ili kulinda, kuepusha
madhara na kufanya mipango endelevu ya sekta hii kwa pamoja” alisema Waziri Mbarawa.
Waziri Mbarawa amebainisha miongoni mwa matumizi hayo yasiyo sahihi ni pamoja na ujenzi holela wa minara na majengo marefu karibu na viwanja vya ndege ambayo yanakuwa ni vikwazo vya kiusalama katika shughuli za Usafiri wa Anga hususan ndege.
“Ni
muhimu tukafahamu kuwa hata shughuli za kijamii zilizopo kwenye maeneo
yanayozunguka viwanja vya ndege zinaweza kuathiriwa. Mfano, uwepo wa
shughuli za shule na hospitali karibu kabisa na kiwanja cha ndege
zinaathiriwa na kelele za milio ya ndege hivyo kusababisha usumbufu
wakati mwingi”amesititiza Mhe.Mbarawa.
Aidha
wa upande wake Mhandisi Kavishe ameongeza kuwa matumizi ya ardhi yasiyo
sahihi yanaweza kuleta hatarishi ya ajali kwa ndege akitolea mfano
uwepo wa jalala au madimbwi makubwa ya maji ni kivutio cha wanyama na
makundi makubwa ya ndege ambapo kwa wingi wao wanapoivamia ndege ni
hatari siyo tu inayoweza kuleta hitilafu kwenye ndege bali hata
kusababisha ajali.
Ni
wazi kuwa changamoto hii inakuwa kwa haraka na ni matoke ya ukuaji wa
uchumi na maendeleo ndio maana tuko hapa tupate uelewa wa pamoja ili
wakati wa kupanga matumizi ya ardhi basi tujitahidi kuepuka kutengeneza
athari zaidi alisema Mhandisi Kavishe.
Bodi ya Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) iliyoko chini ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi inajukumu la kuratibu na kusimamia ujenzi kwa kusajili wataalam na makampuni ya ujenzi, kukagua miradi ya ujenzi na kutoa mafunzo kwa vitendo kwa watalaam wa ujenzi hapa nchini ambapo zaidi ya Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi 1520 wamesajiliwa.
No comments:
Post a Comment