HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 1, 2021

NHC KUJENGA ENEO LA MRADI WA UJENZI WA OFISI ZA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio (wanne kushoto) akiwa kwenye picha ya Pamoja na Mhandisi kutoka NHC, Mr. Thomas Binnaly (wanne kulia) baada ya kufunga kikao cha cha kumkabidhi Mkandarasi, NHC eneo la Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Wizara kwa awamu ya pili Mji wa Serikali Mtumba.Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio amefungua kikao cha kumkabidhi Mkandarasi, NHC eneo la Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Wizara kwa awamu ya pili Mji wa Serikali Mtumba. Kikao hicho kimefanyika tarehe 30 Septemba 2021, Mtumba, jijini Dodoma.

 Kadio amesema Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inamshukuru Mhe.  Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuipa wizara fedha kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ambazo zitawezesha wizara kuwa na           ofisi  za kutosha.
Mshauri Elekezi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Peter Salyeem, akisoma ajenda za kikao kabla ya kumkabidhi Mkandarasi, NHC eneo la Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Wizara kwa awamu ya pili Mji wa Serikali Mtumba.
Baadhi ya Watendaji walioshriki katika kikao cha kumkabidhi Mkandarasi, NHC eneo la Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Wizara kwa awamu ya pili Mji wa Serikali Mtumba.
Mshauri Elekezi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Peter Salyeem akionyesha eneo la Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Wizara kwa Mkandarasi, NHC na baadhi ya Watendaji kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad