IDADI kubwa ya Wananchi wa jiji la Dar es salaam wamejitokeza kupima afya zao kupitia Kampeni ya Afya Kwanza yenye kauli mbiu ya Shtukia Fasta inayoendeshwa mjumuiko wa Taasisi za kijamii mbalimbali kwa ushirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika dhamira ya kuondoa tatizo la Saratani Nchini Tanzania.
Hatua hiyo imekuja kufuatia maadhimisho ya mwezi wa magonjwa ya Saratani Duniani.Taasisi
hizo ambazo ni Pamoja na Inspire Consultants, Associazione Ruvuma
Onlus, Shujaa Cancer Foundation, Genesis Cancer and Palliative Care
Foundation,
Tanzania
Comprehensive Cancer Project, Ocean Road Cancer Institute na kituo cha
matangazo Clouds Media Group zimekuja Pamoja kuadhimisha mwezi huu kwa
kujitoa, kuweka kambi kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya kutoa huduma
ya upimaji bure bila malipo, kwa wakazi wa maeneo mbalimbali jijini Dar
es Salaam.
Akizungumza
katika ufunguzi wa kambi ya kwanza ya siku mbili ya upimaji bure
Mbagala, mtaalam kutoka Taasisi ya Tanzania Comprehensive Cancer
Project, TCCP, Dr Irene Ketegwe amesema zoezi hili linatazamiwa
kupunguza gharama kubwa inayoweza
kuingiza
nchi kutokana na ugunjwa huu kuchelewa kugunduliwa mapema ikiwa ni
pamoja na kupunguza idadi ya watu kupoteza Maisha.Dr. Irene Katemwa,
ameeleza kuwa matibabu ya Saratani ya Matiti hutolewa kulingana na hatua
za ugonjwa na hali ya mgonjwa. Amesema huduma za matibabu hutolewa kwa
njia ya upasuaji katika hatua za mwanzo za
ugonjwa,mionzi,Dawa
za Saratani au mionzi na dawa kwa Pamoja na ambazo gharama zake huwa
mara dufu endapo mgonjwa anapochelewa kugundulika mapema.Vilevile
amesisitiza kuwa wanawake wanapoona dalili zifuatazo:- kutokwa na damu
baada ya kujamiana, kutokwa na uchafu sehemu za siri,kutokwa na majimaji
yenye
harufu
mbaya,kutokwa na usaha sehemu za siri,kutokwa na damu sehemu za siri
isiyo na hedhi,maumivu ya kiuno na maumivu ya tumbo chini ya kitovu
wawahi Hospitali kwani hizo ni dalili za Saratani ya Mlango wa kizazi.
Katika zoezi hilo Mtaalamu kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road Dr Crispin Kahesa amesema‘‘Saratani
ya Mlango wa kizazi ni Saratani inayoongoza kwa vifo vingi vya wanawake
hapa Tanzania hivyo utaratibu wa kupima inasaidia kupunguza vifo hivyo
kwani Saratani hii ikigundulika mapema inatibika’’.
Wananchi
waliojitokeza kupima wameshauriwa kuendelea kuchukua tahadhari za
kujikinga na ugonjwa huo kwa kutojamiana na wanaume wengi kwani kirusi
cha ugonjwa huo kinasambaa kwa njia ya kujamiana na mtu mwenye kirusi
hicho, hivyo wanawake wameshauriwa kupenda na kulinda Afya zao.
Akieleza
juu ya uitikiwaji wa kampeni hii ya Afya Kwanza yenye kaulimbiu ‘stukia
Fasta’, Bi Happy Seiph Rwechungura mratibu wa zoezi hili alisema
wananchi wengi wameamka na kuona umuhimu wa wajitokeza kupima afya zao.
Amesema
“tunaowakuta na matatizo tunawapa barua ya kwenda Taasisi ya Saratani
Ocean Road ili kuendelea kupata uchunguzi na tiba endelevu,”Baadhi ya
wakazi wa Mbagala, Tabata, Kigamboni waliojitokeza katika kambi ya
upimaji kwa ajili ya kupima viashiria vya saratani ya matiti, mlango wa
kizazi na tezi dume waligundulika na viashiria waliweza kupatiwa rufaa
ya kwenda kupima zaidi kwenye Taasisi ya SaratanI Ocean Road jijini Dar
es salaam.
Wakazi
wa maeneno mengine jijini Dar es salaam wameombwa kufuatilia zoezi hili
la upimaji bila malipo katika kambi nyingine zinazoendela hapa jijini
dar es salaam hadi kufikia tarehe 29 mwezi oktoba 2021. Vituo
vilivyobaki ni Kimara Stop Over tarehe 25 na 26 pamoja na Tanganyika
Packers, Kawe tarehe 28 na 29 Oktoba 2021.
Huduma
zinazoendelea kutolewa ni pamoja na upimaji wa tezi dume, saratani ya
matiti na saratani ya mlango wa kizazi.Mmoja wa wanufaika wa huduma ya
upimaji wa saratani ya matiti na mlako wa
kizazi, Bi Fatuma Mikidadi amesema huduma hiyo ni nzuri na kuomba muda
uongezwe.
“Huduma
ni nzuri lakini siku mbili hazitoshi kwa sababu watu ni wengi na
wengine bado hawana taarifa hivyo wakisikia watakuwa wengi,” amesema
Mileka
Akiongea
kutoka Mbagala Zakhiem zoezi hili lilipoanzia Mmoja wa madaktari
wanaotoa huduma kutoka mradi wa TCCP amesema hadi kufikia saa nne tayari
walikuwa wameshawaona wagonjwa zaidi ya 300 na kwamba kutokana na wingi
wa watu wanakusudia kuwahudumia hadi watu 3000 kwa muda wa siku 10.
“Tulianza
shughuli saa moja lakini hadi kufikia saa 4:30 asubuhi tumeshaandikisha
wagonjwa zaidi ya 300 kwa siku hizi mbili tunaweza kuwaona wagonjwa 600
kutokana na idadi ya watu kuwa kubwa, na uwezo wetu kwa eneo hili”
amesema mratibu mwandamizi wa Mradi, Bi Nseya Kipilyango kutoka Taasisi
ya Inspire Consultants.
Amesema
katika idadi ya watu waliojitokeza wengi ni wanawake lakini hata hivyo
wameshangazwa na idadi kubwa zaidi ya wanaume hasa ukichukulia kuwa
kutokana na dhana potofu kuhusu upimaji mwanzaoni wanaume wengi
waliogopa kujitokeza, alisema lakini baada ya uelimishaji unaondelea
katika kituo cha matangazo Clouds Media Group elimu hii imesaidia
kuongeza idadi hiyo yawanaume kushiriki katika zoezi la upimaji wa tezi dume ambao hufanyika kwa njiaya damu.
“Tunashukuru
serikali kwa kutupatia maeneo mazuri kwa ajili ya kutoa huduma
hizi,changamoto kubwa tuliyokutana nayo ni utoaji wa huduma hii
kulingana na watu wanaojitokeza, bado uhitaji ni mkubwa na uwezo wetu ni
mdogo, tunaomba watu na taasisi mbalimbali kujitokeza kuchangia zoezi
hili ili tuweze kufikia watu wengi zaidi.”
Waandaji
wa zoezi hili wameomba msaada Pamoja na pesa taslimu wananchi na
makampuni wanaweza kuchangia ili zoezi hili lifanyike Nchi nzima bila
malipo.
“Tuna
uhitaji mkubwa sana wa PSA Kits kwa wanaume kupima kwa njia ya damu,
tents za wagonjwa kusubiri, Tunahitaji wataalamu wa Ultrasound , medical
doctors na manesi kupunguza gharama za uendeshaji
Wakujitolea ili mapambano yawe endelevu kuisaidia serikali kupambana na Saratani” alisema Dr Irene Ketegwe.
No comments:
Post a Comment