HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 12, 2021

KONGAMANO LA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA MISITU KUFANYIKA IRINGA NOVEMBA 10 HADI 12 MWAKA 2021.

 

 Mkoa wa Iringa ambao una miliki 40% ya misitu ya nchini Tanzania unatarajiwa kufanya Kongamano kubwa la wawekezaji na wadau wa sekta ya misitu tarehe 10 hadi 12 Novemba 2021. Akizindua    maandalizi ya Kongamano hilo Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh Queen Sendiga alisema ‘’ Mkoa wa Iringa ni kinara wa sekta ya misitu, na sasa Serikali ya Mkoa wa Iringa baada ya kuzindua mwongozo wa uwekezaji wa Mkoa wa Iringa mwanzoni mwa mwaka 2021, sasa tunaleta kwenu kongamano hili la uwekezaji katika sekta ya misitu ambalo litaenda sambamba na maonesho ya sekta ya misitu na pia kongamano la wadau wa sekta hii’’.

  Aliendelea kusema ‘’ pamoja na Mkoa wa Iringa kuwa kinara wa Sekta ya misitu lakini bado kuna fursa pana za uwekezaji na uanzishaji wa biasahra au huduma kwenye sekta ya misitu, Wilaya zote za Mkoa wa Iringa zimetenga aridhi kwa ajili ya uwekezaji katika sekta ya misitu hivyo Twenzetu Iringa, Misitu inalipa , Wekeza Sasa.’’ Alimalizia kwa kusema tunatarajia Waziri Mkuu Mh Majaliwa Kassim Majaliwa kuwa mgeni rasmi kwenye Kongamano hili la Uwekezaji katika sekta ya misitu. Kujisajili kwa ajili ya kongamano hili bonyeza link hii https://www.forestryinvestmentforum.co.tz.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh Queen Sendiga akizungumza baada wa kuzindua  maandalizi ya kongamano la uwekezaji kwenye sekta ya misitu. Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mh Saady Mtambule , Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Mohamed Moyo na kushoto kwa Mkuu wa Mkoa ni Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mh Peres Magiri

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh Queen Sendiga akizungumza wakati wa uzinduzi wa maandalizi ya kongamano la uwekezaji kwenye sekta ya misitu.

 

 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad