HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 24, 2021

RAIS WA ZANZIBAR AFUNGUA MJADA WA UWEKEZAJI WA BIG BREAKFAST HOTELI YA VERDE MTONI ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa Tuzo Maalum ya Kuhamasisha Uwekezaji Zanzibar Namba Moja, akikabidhiwa na Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Kazi Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Mhe. Mudrik Ramadhan Soraga, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mjadala wa Uwekezaji wa Big Breakfast, uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Verde Mtoni Zanzibar.(Picha na Ikulu)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia wadau wa Uwekezaji Zanzibar wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mjadala wa Uwekezaji wa Big Breakfast, mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Verde Mtoni Zanzibar.

Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi Cheti cha udhamini Meneja Uhusiano Bima Benki ya CRDB –Zanzibar Bi. Hamida Juma, wakati wa hafla ya ufunduzi wa mkutano wa Mjadala wa Uwekezaji wa Big Breakfast, uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Verde Mtoni Zanzibar.

Mtangazaji wa Kituo cha TV cha Clouds 360 Paul James akiongoza Mada ya kwanza kuzungumzia Fursa ya Uwekezaji Zanzibar, katika Mjadala wa Big Breakfast uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Verde Mtoni Zanzibar na (kushoto) Watoa Mada Bi. Victoria Kamazima Wakali wa Kijitegemea, Mkurugenzi Mtendaji wa ZIPA Ndg. Sharif Ali Sharif na Ndg. Masoud Salim Wakili wa Kijitegemea.(Picha na Ikulu)
Mkurugenzi Mtendaji wa ZIPA Ndg. Sharif Ali Sharif akitowa Mada kuhusiana na Fursa za Uwekezaji Zanzibar, wakati wa Mjadala wa Big Breakfast uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Verde Mtoni Zanzibar, uliofunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) na (kulia) Bi, Victoria Kamazima na (kushoto) Ndg. Masoud Salim.(Picha na Ikulu)

Washiriki wa Mjadala wa Uwekezaji wa Big Breakfast wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia na kufungua Mjadala wa Uwekezaji wa Big Breakfast uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Verde Mtoni Zanzibar.(Picha na Ikulu)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akifuatilia Mjadala kuhusiana na Fursa ya Uwekezaji Zanzibar, ikiwasilishwa Mada hiyo na Mkurugenzi Mtendaji wa ZIPA Zanzibar Ndg. Sharif Ali Sharif (hayupo pichani) na (kulia kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Kazi Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Mhe. Mudrik Ramadhan Soraga, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Verde Zanzibar.(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad