HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 29, 2021

MO DEWJI ATANGAZA KUKAA PEMBENI YA UONGOZI SIMBA SC, AMTEUA "TRY AGAIN"


 MWEKEZAJI na Mwanahisa wa Klabu ya Simba SC, Mohammed Dewji (MO Dewji) ametangaza kuachia ngazi katika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi wa Wakurugenzi wa Klabu hiyo badala yake amemtaja Makamu Mwenyekiti, Salim Abdallah (Try Again) kuwa mrithi wake.

MO Dewji ametangaza kuachia nafasi hiyo mapema leo kupitia ukurasa wake rasmi Instagram kwa kuweka kipande kifupi cha video kikimuonesha akitoa kauli hiyo. Amesema amefanya uamuzi huo kutokana na yeye muda mrefu kusafiri nje ya nchi.

 “Makubaliano yaliyofikiwa Septemba 21, 2021 tukikubaliana kuwa Mwenyekiti wa Bodi uwepo wake muda wowote katika kuiongoza Klabu ni muhimu, hivyo kwa makubaliano hayo namteua Salim Abdallah kuanzia sasa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Simba SC”, amesema MO Dewji.

Pia amesema licha ya kuachia ngazi katika nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa Bodi ataendelea kuwa Mwekezaji na Mwanahisa, amesema na kuahidi ataendelea kuipenda Simba SC hadi siku ya kufa kwa muda wote.

“Katika kipindi cha miaka minne nikiwa Mwenyekiti wa Bodi tumefanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na tumepata mafanikio ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mara nne na kufanya vizuri katika Michuano ya Kimataifa ya Ligi ya Mabingwa Afrika, natoa Shukran kwa Viongozi wa Simba, Wanachama na Mashabiki”, ameeleza MO Dewji.

Hata hivyo, MO Dewji amesema Salim Abdallah (Try Again) ana uzoefu wa kazi hiyo kutokana na kufanya kazi kwa ushirikiano wakiwa wote kama Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bodi, ameahidi kushirikiana naye katika nafasi hiyo sambamba na Uongozi wote wa Simba SC.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad