BODI
ya wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB,) imeandaa Semina ya 23
'Research Workshop' na kutoa mafunzo maalumu ya kuwandaa wanafunzi wa
Bodi wanaotarajiwa kufanya tafiti kabla ya kuhitimu mafunzo kutoka bodi
hiyo yaliyoanza leo Sepitemba 27 hadi Oktoba 01, 2021.
Akizungumza
wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
hiyo Godfrey Mbanyi amesema kuwa moja ya matakwa ya CPSP ni kufanya
'Research Paper' na mwanzo wake ni huo kwa wanafunzi kuhudhuria semina
na kupata mafunzo yatakayowapitisha kwa usahihi katika safari yao ya
kufanya tafiti na kuhitimu vyema mafunzo hayo kwa mujibu wa bodi hiyo.
Mbanyi
amesema, katika mafunzo hayo wanafunzi watapitishwa katika maeneo
tofautitofauti ya mbinu za utafiti na andiko la utafiti pamoja na
kuwajengea uwezo wa kuandika tafiti na ripoti mbalimbali kwa kufuata
kanuni na miongozo ya PSPTB katika tafiti zao watafazozifanya.
Aidha
amesema kupitia mafunzo hayo wanafunzi wataelekezwa na kujengewa uwezo
wa jinsi ya kuandaa andiko la utafiti hususani ya PSPTB ili waweze
kuhitimu mafunzo hayo na kuwataka wanafunzi hao kuzingatia umuhimu wa
mafunzo hayo muhimu katika tafiti zao watakazozianza mara baada ya
mafunzo hayo.
''Baada
ya kuhitimu mafunzo haya ya siku tano wahitimu mtapewa vyeti vya
kuonesha ushiriki wenu katika mafunzo haya na kuanza kuandika research
proposal/ mapendekezo ya tafiti zenu mapema iwezekanavyo.'' Amesema.
Mafunzo
hayo ya siku 5 yaliyoanza leo yamewakutanisha wanafunzi zaidi ya 100
kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania ikiwemo Moshi, Mtwara, Mwanza na
wenyeji Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB),
Godfred Mbanyi akizungumza wakati wa kufungua semina ya 23 'Research
Workshop' yenye lengo la kutoa mafunzo maalumu ya kuwandaa wanafunzi wa
Bodi wanaotarajiwa kufanya tafiti kabla ya kuhitimu mafunzo kutoka bodi
hiyo yanayofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es
Salaam leo.
Baadhi
ya wanafunzi wa Bodi wanaotarajiwa kufanya tafiti wakifuatilia hotuba
ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na
Ugavi(PSPTB), Godfred Mbanyi alipokuwa anafungua mafunzo hayo
yanayofanyika kwa siku tano katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini
Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB),
Godfred Mbanyi akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa Bodi
wanaotarajiwa kufanya tafiti waliofika kwenye semina iliyoandaliwa na
Bodi hiyo iliyofanyika leo katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini
Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment