Na Sabiha Khamis Maelezo
Waziri
wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui
ameahidi kudumisha ushirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
na Serikali ya Jamuhuri ya watu wa China ili kuinua Uchumi wa Nchi.
Akizungumza
na Balozi Mdogo wa China aliopo Zanzibar na ujumbe wake, wakati
akipokea msaada wa Dawa kutoka Serikali ya Jamuhuri ya watu wa China Mh.
Mazroui alisema Serikali hizi mbili ni marafiki wa muda mrefu hivyo
wataendeleza ushrikiano huo ili kuwapatia wananchi huduma bora za afya.
Aidha
amesema Serikali ya Zanzibar inaishukuru Serikali ya Jamuhuri ya watu
wa China kwa kushirikiana nao kwa kila hali pamoja na kuwapatia misaada
mbali mbali ikiwemo Dawa, Madaktari na Chanjo ya UVIKO-19.
“Tunishukuru
Serikali ya Jamuhuri ya watu wa China wamekuwa wakishirikiana na sisi
kwa kila hali hususani Wizara ya Afya kwa kutupatia madaktari kila mwaka
na misaada mbali mbali ambayo husaidia katika kutoa huduma kwa
wananchi” alisema Waziri.
Mapema Waziri Mazrui alifafanua kuwa
Wizara yake imepokea Dawa 165 zenye thamani ya takribani Shilingi
Milioni 120 kwa Unguja ambazo ni idadi sawa na Dawa zilizotolewa
Kisiwani Pemba.
Kwa upande wake Balozi Mdogo wa China aliopo
Zanzibar Zhan Zhisheng amesema Serikali ya watu wa China inaahidi
kuendelea kuisaidia Zanzibar kwani tayari wameshajaza mkataba wa kujenga
nyumba za wafanyakazi katika Hospitali ya Abdalla Mzee iliopo Mkoani
Pemba.
Hata hivyo Balozi Zhan amefurahishwa na mashirikiano
yaliyopo baina ya madaktari wa Zanzaibar na madaktari kutoka China
katika utendaji wa kazi unaopelekea kubadilishana Ujuzi katika
utekelezaji wa majukumu yao.
Makabidhiano hayo ya Dawa baina ya
Wizara ya Afya Zanzibar na Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China
yalifanyika katika Ukumbi wa mikutano Hospitali ya Mnazi Mmoja Mjini
Unguja.
No comments:
Post a Comment