HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 14, 2021

TAASISI YA PLPDF YAZINDUA KAMPENI YA KUCHANGIA UJENZI WA VYOO RAFIKI KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU, WAOMBA KUWAUNGA MKONO

 

Mkurugenzi Mtendani wa Taasisi ya Peace Life for Person with Disability Foundation (PLPDF), Sophia Mbeyela akizungumza wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa vyoo rafiki kwa wanafunzi wenye Ulemavu mashuleni leo Julai 14,2021. Kulia ni balozi wa kampeni ya Vyoo rafiki Mlinzi wa Afya yangu, Lita Paulsen.Mkurugenzi Mtendani wa Taasisi ya Peace Life for Person with Disability Foundation (PLPDF), Sophia Mbeyela, Lita Paulsen wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi pamoja na wadau wa maendeleo ya wanafunzi wenye ulemavu mara baada ya kuzindua kampeni ya ujenzi wa Vyoo rafiki kwa wanafunzi wenye ulemavu mashuleni. Kampeni hiyo imeziduliwa leo jijini Dar es Salaam.

 Balozi wa kampeni ya Vyoo rafiki Mlinzi wa Afya yangu, Lita Paulsen akizungumza wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa vyoo rafiki kwa wanafunzi wenye Ulemavu mashuleni leo Julai 14,2021 jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja.

Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii
TAASISI ya Peace Life for Person with Disability Foundation (PLPDF) yazindua kampeni ya ujenzi wa vyoo rafiki kwa wanafunzi wenye Ulemavu mashuleni leo Julai 14, 2021 katika mgahawa wa Lavent Masaki jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi Mtendani wa Taasisi ya Peace Life for Person with Disability Foundation (PLPDF), Sophia Mbeyela Maarufu kama Madam Sophy amesema kuwa vyoo rafiki ni Mlinzi wa Afya hivyo ameiomba serikali na jamii kwa ujumla kuunga mkono kampeni hiyo kwa kuchangia katika Ujenzi wa vyoo mashuleni kwaajili ya matumizi ya wanafunzi wenye ulemavu.

Amesema kuwa Unaweza kuchangia kupitia namba ya M-Pesa 55557777 huku namba ya Akaunti ya Benki ya NMB 22510027964 kwa jina la PLPDF.

"Lengo la kuzindua kampeni hii ni kutaka kujenga vyoo rafiki kwa wanafunzi wenye ulemavu, kampeni hii itakuwa endelevu kwani tumeona changamoto ya vyoo rafiki mashuleni, tunataka wanafunzi walemavu walio mashuleni wasome bila kuwa na changamoto.

Changamoto hii nimeona katika shule ya Sekondari Jangwani nilitembelea nakuona vyoo vichache na wanafunzi ni wengi, Kama Jangwani ambayo ipo Mjini inachangamoto ya vyoo rafiki kwa wanafunzi, je huko vijijini itakuwaje?" Amehoji Sophia.

"Ukubwa wa Changamoto hii tumeanza kuona katika shule ya sekondari ya Jangwani ambapo kunawanafunzi 84 lakini kunamatundu ya choo ambayo ni rafiki ni manne (4) tuu. Lakini katika manispaa ya Ilala ina shule 17 zenye wanafunzi mchanganyiko na wanafunzi wenye ulemava lakini hazina vyoo rafiki kwa wanafunzi hao." Amesema Sophia

Hata hivyo Sophia amesema kuwa anaungana na wadau wengine wa afya na maendeleo kwaajili kuchangia ujenzi wa vyoo katika manispaa ya Ilala katika shule ya Sekondari ya Jangwani jiji la Dar es Salaam pia ujenzi wa vyoo rafiki kwa walemavu utaendelea katika mikoa mingine.

Licha ya hayo amesema kuwa kama kampeni hiyo itafanikia zaidi katika mkoa wa Dar es Salaam kampeni hiyo itaendelea katika shule nyingine katika wilaya nyingine hapa nchini na baadae tutendelea kutoa elimu jumuishi kwa wanafunzi walemavu juu ya suala la kuwa na vyoo rafiki kwa mahitaji ya wanfunzi wenye ulemavu.

Amesema kuwa watahakikisha wanafunzi wenye ulemavu wanasoma katika mazingira mazuri, hiyo wanaomba wadau, serikali pamoja na jamii kwa ujumla kuweza kuungana na Taasisi ya Peace Life for Person with Disability Foundation (PLPDF) katika kufanikisha lengo la kuwasaidi wanafunzi wenye ulemavu walioko mashuleni ili wapate elimu bora katika mazingira mazuri zaidi.

Kwa Upande wa mgeni Rasmi ambaye ni balozi wa vyoo rafiki  mlinzi wa afya yangu, Lita Paulsen amesema ameisa jamii kuunga mkono kampeni ya Sophia kwaajili ya kusaidia wanafunzi wenye ulemevu mashuleni.

Amesema kuwa sio lazima mtu achangie pesa bali anaweza kuchangia mawazo au vitu vitakavyowezesha kujenga vyoo rafiki kwa watu wenye ulemavu. Madam Lita amesema kuwa choo kimoja kinagharimu shilingi milioni sita hadi saba tuu hivyo amewaomba wadau kujitoa kwaajili ya hilo ili kuwezesha wanafunzi wenye ulemavu waweze kufikia malengo yao.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam, Kagemulo Runyoro amesema kuwa serikali imetoa ushirikiano wa hali ya juu kwa kutoa eneo ambalo litakwenda kujengwa vyoo rafiki kwa waafunzi wenye ulemavu pia na vibali vingine vyote ambavyo vitatakiwa.

Amesema kuwa pia watajitahidi kutafuta wadau katika kuchangia kampeni ya kujenga vyoo rafiki kwa wanafunzi wenye ulemavu mashuleni.

"Nikweli kumekuwa na hali ambayo sio rafiki kwa wanafunzi walemavu hususani majengo, madarasa, ofisi na vyoo zimekuwa sio rafiki kwa watu wenye ulemavu, tutajitahidi kuweka hali nzuri kwa watu wote." Amesema Kagemulo

Nae Mwali Chavala Mariam amesema kuwa Miundombinu katika shule ya Sekondari Jangwani kwa wanafunzi wenye ulemavu sio rafiki  pamoja na mahitaji mengi waliyonayo na changamoto walizonao, choo ni kitu mhimu zaidi ili mtu aishi salama na kwa afya yake.

"Sisi tunatoa wito kwa taasisi mbalimbali mashirika mabalimbali, makampuni na serikali kila mtu aguswe aone kwamba leo ama kesho anamtoto mlemavu tuchangie ili watoto hawa wajengewe vyoo ambavyo ni rafiki kwao." Amesema Mwalimu Chavala.

Hata hivyo Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Jangwani, Aisha Ahmed amesema kuwa kampeni hii itakavyofanikiwa itasaidi wanafunzi wengi zaidi wenye ulemavu. "Itatatua changamoto zilizopo za vyoo rafiki katika shule na sisi tutazidi kupata maarifa ya elimu bila kikwazo na kuweza kuwa na usiri pale tutakapokuwa na shida ya kwenda chooni."

Pia ameiomba Serikali na mashirika yasiyoyakiserikali na yakiserikali kuchangia kampeni iliyoanzishwa na Sophia kwaajili ya kusaidi watu wenye ulemavu hapa nchini ili wanafunzi wenye ulemavu kupata elimu bila vikwazo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad