HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 14, 2021

DC AWAPONGEZA WANANCHI LIGERA KUANZISHA UJENZI WA BWENI LA WANAFUNZI

 

 NA YEREMIAS  NGERANGERA…NAMTUMBO

Mkuu  wa wilaya  ya Namtumbo  mkoani Ruvuma  Julius  Ningu ameupongeza  uongozi wa kata ya ligera  kwa kuhamasisha wananchi  wa kata hiyo  kutumia nguvu zao  kuanzisha  ujenzi  wa bweni  la wanafunzi wa kike  ili kupunguza adha ya wanafunzi hao  kutembea umbali mrefu  kuhudhuria masomo .

Akiongea  na wajumbe wa kamati  ya  ujenzi  wa shule  ya Sekondari , wajumbe wa kamati  ya   maendeleo ya  kata, walimu  wa shule ya sekondari  Lukimwa  pamoja na watendaji wa  vijiji wa  kata hiyo  Mkuu  wa wilaya hiyo aliwapongeza  kwa jitihada ya kuhamasisha  wananchi  juu ya ujenzi wa bweni  la wasichana katika shule ya sekondari Lukimwa.

Aidha  Ningu  alidai ipo  haja ya viongozi  kushirikiana ,kushikamana  na kuwa na hoja ya pamoja  ya kusimamia shughuli  za maelendeleo  na kuongeza  uwazi  katika matumizi ya fedha  zinazotumika ili kuondoa  malalamiko  yanayoweza  kuibuka .

Diwani wa kata ya Ligera bwana Sambode  Mhongo  alimhakikishia mkuu wa wilaya hiyo kuwa  ujenzi wa  bweni la wasichana katika shule ya Sekondari  Lukimwa uliibuliwa kwenye kikao cha maendeleo ya  kata hivyo  ushirikishwaji  wa viongozi  na wananchi  ni mkubwa  ,uwazi wa matumizi ya fedha  nao ni mkubwa  .

Pamoja  na  mambo mengine  Mhongo  alisema wananchi kwa uwezo wao kupitia vikao vya kisheria maendeleo ya kata  walisema  wapo tayari  kujenga  bweni hilo kwa kutumia nguvu zao  mpaka hatua ya boma  lakini  pamoja na maamuzi hayo  akaomba pia watu wenye mapaenzi mema  ya kuunga juhudi zinazofanywa na wananchi hao kuchangia  juhudi hio .

Kaimu mkuu wa shule ya sekondari  Lukimwa bwana  Kassian Lwehela  alimwambia mkuu wa wilaya ya Namtumbo  kuwa  ushirikishwaji  wa  viongozi  ,wananchi  katika maswala yote yanayohusu  shule hiyo ni mkubwa  kwani kila jambo linaloamliwa  katika vikao mihutasari ya vikao huandikwa  na huwekwa kwa kumbukumbu alisema  Lwehela.

Mkuu  wa wilaya ya Namtumbo  alifanya ziara ya kikazi  katika shule ya sekondari  ya Lukimwa kukagua  utendaji kazi ,usimamizi wa miradi ya ujenzi  wa maabara  , bweni  pamoja na kusikiliza changamoto  zinazoikabili shule hiyo na kuzitafutia ufumbuzi  huku akiwapongeza  kwa  kuanzisha  ujenzi wa bweni  la wasichana wa shule hiyo .


 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad