HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 21, 2021

Watalii wajitokeza kuona maajabu ya jiwe la ekari 7.5 lenye ramani ya bara la Afrika juu yake

 

 Na Amiri Kilagalila,Njombe

Baada ya jitihada kubwa zinazofanya na serikali katika kuvitangaza vivutio vya utalii ndani na nje ,Huko mkoani Njombe jiwe la kushangaza lenye ukubwa wa ekari 7.5 likiwa na umbo la ramani ya bara la Africa juu yake huku muonekano wa nje wa jiwe zima ukiwa na umbo la ramani ya Dunia limegeuka kivutio kikuu cha utalii mkoani humo na kusababisha mamia ya watu kuendelea kufika katika kijiji cha Igodivaa wilayani Wanging'ombe kujionea maajabu hayo ya kivutio hicho

Jiwe hilo ambalo limepewa jina asilia la Lwivala likimanisha uangavu lina mambo mengine matano yakustaajabisha ikiwa ni pamoja na kuwa na mkanda wa mwamba ambao unadaiwa kuwa ni mlango wa kuzimu,Nyoka mkubwa asiye na madhara kwa viumbe wengine,kochi asilia la kifalme,Kisima kilicho katikati ya mwamba ambacho hakikauki kipindi chote cha mwaka pamoja na viji mwamba vidogo vinavyo ng'ara kila ifikapo saa 12 asubuhi na jioni.

Kwa mara ya kwanza Mwamba wa Lwivala ulitambuliwa 1996 na kutangazwa 2002 na mwenge wa uhuru kuwa kivutio cha utalii na kuanzia hapo maelfu ya watu kwa nyakati tofauti waka anza kuzuru kujionea maajabu hayo ambapo mingoni mwao ni Hannes Van Niekerk raia wa Afrika kusini,Helen Mlowe na Justin Mligo ambao wameeleza namna walivyofurahia kutembelea kivutio hicho.

"Kwanza eneo hili linavutia na kila mtu atakayefika hapa tunaamini atavutiwa na mazingira haya,lakini inabidi tuvitunze vifutio hivi,tumeona picha ya bara la Afrika juu ya jiwe ambapo sijawhi ona maajabu kama haya"alisema Heln Mlowe

Ikielezwa historia fupi ya jiwe hilo na Mzee wa mila ambaye pia ni muongoza wageni Yuda Masamaki Mlowe  na Sebastian Anania mwenyekiti wa kijiji cha Igodivaa wanasema katika jiwe hilo ndipo walikuwa wanakutana zamani na kuomba mambo mbalimbali na kujibiwa lakini kwasasa imekuwa ngumu kwasababu ya shamabulio la tamaduni za magharibi.

"Siku za nyuma tulikuwa tunaleta magari yakawa yanaingia mpaka huku kwa hiyo maji yalizila na wenye mizimu yao kwa hiyo lazima tuhakikishe haya tunayafanyia kazi"alisema Yuda Mlowe

Wakati mwamko wa utalii ukizidi kukua kila uchwao lakini vivutio vingi vya mkoa wa Njombe havijulikani jambo ambalo linamsukuma mkurugenzi wa kampuni ya RAMIKA Safari's and Tours Michael Katona kujitosa huko na kuanza kuvitangaza na kuhamasisha watu kutembelea

"Vivuti vya ndani ya mkoa wa Njombe watu wengi wamekuwa hawavitambui na wengine wanavishangaa kwa hiyo sisi wadau wa utalii ndani ya mkoa wa Njombe na nyanda za juu kusini tumeona angalau sasa tuhamisishe jamii kuona umuhimu wa hivi vivutio"alisema Michael Katona
Baadhi ya watalii wa ndani na wa nje wakiwa wamezunguka picha ya ramani ya bara la Afrika ambayo ipo juu ya jiwe lenye ukubwa wa ekari 7.5 wakipewa maelekezo na msimamizi wa kivutio hicho wilayani Wanging'ombe mkoani Njombe.
Baadhi ya watalii wa wakiwa wamekaa kwenye mfano kochi la asili (Jiwe) lilopo kwenye kivutio cha jiwe huku lenyewe likiwa na historia yake katika kivutio hicho.
Baadhi ya watalii wakipata maelekezo kabla ya kuanza kuzunguka kivutio cha jiwe la Lwivala mkoani Njombe.



 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad