HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, May 19, 2021

PAKISTAN, IRAN ZAAHIDI KUIMARISHA DIPLOMASIA YA UCHUMI

 

Na Mwandishi wetu

Pakistan na Iran zimeahidi kuendelea kuimarisha diplomasia ya uchumi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maslahi mapana ya pande zote.

Ahadi hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti wakati Mabalozi wa Pakistan na Iran walipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Mabalozi waliokutana na Waziri Mulamula ni Balozi wa Pakistani hapa nchini Mhe. Mohammad Saleem pamoja na Kaimu Balozi wa Irani hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh ambapo viongozi hao wamejadili masuala ya kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Nchi zao lakini pia kuimarisha na kuboresha diplomasia ya uchumi kwa maslahi mapana ya nchi zote.

Pamoja na mambo mengine, Balozi wa Pakistan Mhe. Saleem ameelezea kufurahishwa na uhusiano mzuri uliopo baina ya Iran na Tanzania na amepongeza hatua mbalimbali ambazo Serikali ya Tanzania imeendelea kuzichukua katika kuimarisha diplomasia ya uchumi.

Nae Kaimu Balozi wa Iran amesisitiza juu ya uwekezaji na biashara ambapo amesema kuwa Serikali yake ipo tayari kufanya biashara na Tanzania na kuinua uchumi wa wananchi wan chi zote mbili.

Kwa upande wake Balozi Liberata Mulamula (Mb) amewahakikishia mazingira salama ya biashara na uwekezaji na kuwaahidi ushirikiano wa kutosha kutoka Tanzania.

Kadhalika,Waziri Mulamula amesema ushirikiano wa diplomasia ya uchumi kati ya Tanzania na Pakistan unatoa fursa nyingi ikiwemo kukuza biashara hasa katika sekta ya kilimo ikiwemo chai, pamba, korosho, mbegu za mafuta, Madini ya Tanzanite, pamoja na uwekezaji.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimkaribisha Balozi wa Pakistan hapa nchini Mhe. Mohammad Saleem pamoja na ujumbe wake katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam
Balozi wa Pakistan hapa nchini Mhe. Mhe. Mohammad Saleem akiongea jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam
Balozi wa Pakistan hapa nchini Mhe. Mohammad Saleem akimuonesha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula takwimu za ukuaji wa biashara kati ya Pakistan na Tanzania katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimkaribisha Kaimu Balozi wa Iran hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam
Kaimu Balozi wa Iran hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh akimuelezea jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimueezea jambo Kaimu Balozi wa Iran hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam
Kikao kikiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na Balozi wa Pakistan hapa nchini Mhe. Mohammad Saleem pamoja na baadhi ya maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ubalozi wa Pakistan


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad