HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 8, 2021

WAZIRI ATAKA WALIMU KUCHANGAMKIA FURSA

 

 

Waziri ataka waalimu kuchangamkia FURSA. Sekta ya benki imepiga hatua kubwa sana Nchini Tanzania kwenye miaka ya 2000. Umuhimu wa sekta hii ndio ulimpelekea Waziri Suleiman Jafo kuwataka waalimu Nchini Tanzania kuchangamkia FURSA ya mikopo na huduma ya benki yao ya Mwalimu commercial bank ambayo sasa inawawezesha kupata huduma kupitia matawi, ATM, Mwalimu Wakala na Mwalimu mobile popote Tanzania. Akizungumza wakati wa kuzindua huduma ya Mwalimu Visa Card Waziri Jafo alisema kwa waalimu ambao wanalenga kujikomboa kiuchumi ni vizuri wakatumia huduma za Mwalimu bank kwani sio tu inawapa mikopo nafuu lakini pia inawajali kabla ya ajira na baada ya ajira yaani wakistaafu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad