Na Munir Shemweta, MISUNGWI
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi ameitaka halmashauri ya wilaya ya Misungwi mkoa wa Mwanza kuhakikisha inapanga na kupima maeneo yanayopitiwa na miradi ya kimkakati ya treni ya Mwendokasi (SGR) na Kivuko cha Kigongo katika halmashauri hiyo mkoani Mwanza.
Akizungumza wakati wa ziara yake ya kutembelea maeneo ya miradi ya upimaji katika maeneo ya miradi hiyo leo tarehe 1 Februari 2021 Lukuvi alisema, hakuna kuendeleza maeneo yanayopitiwa na miradi ya SGR na Kivuko cha Kigongo mpaka maeneo hayo yatakapopangwa mpango wa matumizi bora ya ardhi.
”
Maisha lazima yabadilike na msinyang’anye wananchi maeneo yao bali
maeneo hayo yapangwe na kupangiwa matumizi yatakayoendana na hadhi ya
miradi” alisema Lukuvi.
Alisema,
halmashauri ni mamlaka ya upangaji hivyo Misungwi inapaswa kuzuia
kuendelea kwa ujenzi katika maeneo hayo mpaka yapangwe kwa lengo la
kupandisha hadhi na kuwa mji wa kisasa (modern city) ambapo alisisitiza
kuwa haiwezekani kuacha eneo linaloweza kuhudumia takriban nchi tano
likaachwa kiholela.
”
Zuieni maendezo yote kandokando ya daraja ili muyapange vizuri na
wanaotaka kuendeleza mhakikishe wanaendeleza yale yanayoshabihina na
mradi” aliongeza Waziri wa Ardhi.
Aliongeza
kwa kusema kuwa kiasi cha shilingi milioni 300 ilizokopeshwa
halmashauri ya wilaya ya Misungwi na Wizara ya Ardhi kwa ajili ya mradi
wa kupanga, kupima na kumilikisha ziendelee kubaki kwa ajili ya kupanga
maeneo ya mradi na kubainisha kuwa, hata halmashauri hiyo ikihitaji
wataalamu kutoka wizarani kusaidia mradi wa upimaji katika eneo hilo
basi inaweza itapatiwa.
“Lazima
misungwi uwe mji maarufu mtu akitaka kuja kulala aje maana hili ni
daraja la kimkakati litakalohudumia takriban nchi tano, tunataka
satelite city iliyopangwa na itakayokuwa na huduma zote za msingi zenye
hadhi inayofanana na mji huo.
Waziri
wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alitembelea eneo
la mradi wa upimaji katika kitongoji cha Kigongo kilipo kivuko cha
Kigongo (Kigongo Ferry) pamoja na eneo la kimkakati la Fella inapopita
treni ya Mwendokasi ya SGR.
Mkuu
wa Idara ya ardhi katika halmashauri ya wilaya ya Misungwi Fredrick
Nyoka alisema, tayari idara imeanza kazi ya upangaji na kupima maeneo
yanayopitiwa na miradi ya SGR na Kivuko cha Kigongo na tayari baadhi ya
wananchi wameshalipwa fidia na Mamlaka ya Bandari Tanzania huku Shirika
la Reli likitarajiwa kumaliza kuwalipa fidia wananchi mwisho wa wiki
hii.
No comments:
Post a Comment