HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, February 10, 2021

RAIS DK.MWINYI AZUNGUMZA NA WAHARIRI NA WAANDISHI WA HABARI IKULU ZANZIBAR

 

 

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Waandishi wa Habari na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari katika mkutano wake uliofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu jijini Zanzibar.

Mkurugenzi Mkuu wa Channel Ten Jaffar Hanui  kushoto) ( na (kulia) Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa  Kampuni ya Uhuru Media Group ltd Bw. Ernest Sungura, wakifuatilia mkutano wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya habari mbalimbali katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 9-2-2021.

BAADHI ya Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali wakifuatila mkutano wao na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizungumzia mafanikio ya Siku mia moja za Uongozi wake Zanzibar, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

BAADHI ya Wahariri wa vyombo vya habari wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi,(hayupo pichani) akizungumza katika mkutano wake na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

MHARIRI Mtendaji wa gazeti la Nipashe Bi. Beatrice Bandawe na Mhariri wa Clouds Media Joyce Shebe. wakifuatilia mkutano wao na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad