Na Amiri Kilagalila, Njombe
CHAMA kikuu
cha ushirika mkoani Njombe (NJORECU) kinatarajia kuanza upya uchakataji
wa unga wa mahindi kupitia kiwanda kinachomilikiwa na Chama hicho
kilichosimama mwaka 2019 ikiwa ni miezi tisa baadaye mara baada ya
kufunguliwa na kuanza kufanya kazi mwaka 2018.
Meneja
mkuu wa NORECU mkoa wa Njombe Samuel Mlumba,amebainisha hayo katika
mkutano na wanachama uliofanyika mjini Njombe,huku akibainisha kuwa zipo
sababu mbali mbali ikiwemo changamoto za uongozi zilizosababisha
kiwanda hicho kufanya kazi kwa muda mfupi na kutokana kuondoshwa kwa
changamoto hizo hakuna sababu itakayozuia kiwanda hicho cha uchakataji
wa Sembe kuanza kufanya kazi.
Mlumba
amesema Kiwanda kilichopo mjini Njombe kilichosimama March 2019 huku
kikiwa kimefanya kazi miezi 9 tangu kilipoanza kufanya kazi June 2018
kinatarajiwa kuanza uzalishaji kuanzia June mpaka March mwaka wa fedha
wa 2022
“Sababu
zilizopelekea kufanya kazi kwa miezi 9 safari hile sasa hivi
hazipo,kwasababu zilikuwa ni changamoto za kiutumishi na usimamizi wa
kiwanda hicho”alisema Mlumba
Aliongeza
“Tupo kwenye mkakati wa kutafuta wataalamu waweze kututengenezea mpango
biashara kwa ajili ya kiwanda cha kuchakata Sembe”aliongeza Mlumba
Nestory
Betram ni kaimu mhasibu mkuu wa NJORECU,amesema kabla ya kufika mwaka
wa fedha wanatarajia kununua tani za mahindi 1199.7 zenye tahamani ya
shilingi milioni 600 kutoka kwenye AMCOS mbali mbali.
Benedict
Mwageni ni Mwenyekiti wa bodi ya mpito wa chama kikuu cha ushirika mkoa
wa Njombe,ametoa wito kwa wakulima walioko kwenye AMCOS kujiandaa
kunufaika kwa kuwa kiwanda hicho kinaenda kuongeza thamani ya mazao.
“Soko
la kwanza la mahindi la wana Njombe liwe ni Chama kikuu cha ushirika,
kiwanda chetu kitakapoanza kufanya kazi,tunatarajia kila siku kuchakata
Mahindi tani zisizokuwa pungufu ya 15 kwa hiyo kwa mwaka tutakuwa na
kilo 4500”alisema Benedict Mwageni
Romanus
Lugome na Mariana Chaula ni miongoni wa viongozi wa vyama vya msingi
(AMCOS) mkoani Njombe wameshukuru uongozi wa Chama Kikuu kuona namna ya
kufufua matumaini ya muda mrefu ya Chama kundeleza miradi yao ikiwemo
kiwanda hicho kitakachokuwa na msaada kwa wakulima wa Mahindi.
Samuel
Mlumba Meneja mkuu wa NORECU mkoa wa Njombe akieleza namna
walivyojipanga kuendeleza miradi ya Chama ikiwemo uendeleaji wa eneo
lililopo kata ya Mlangali wilayani Ludewa lililotengwa kwa dhumuni la
kujenga kiwanda kingine cha kuchakata Sembe mkoani Njombe.
Baadhi
ya viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS) Katika mkutano mkuu wakiwa
makini kusikiliza ajenda ya fedha na mipango ya Chama kikuu ili
kuimarisha ushirika mkoani humo.
Moja
ya mitambo ya kiwanda cha kuchakata mahindi kinachomilikiwa na NJORECU
kilichopo kata ya Njombe mjini wakati kilipoanza kufanya kazi.
No comments:
Post a Comment