HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, February 5, 2021

Kiwanda kilichofanya kazi miezi tisa na kusimama, kuanza kazi tena kuanzia June 2021

 

Na Amiri Kilagalila, Njombe
CHAMA kikuu cha ushirika mkoani Njombe (NJORECU) kinatarajia kuanza upya uchakataji wa unga wa mahindi kupitia kiwanda kinachomilikiwa na Chama hicho kilichosimama mwaka 2019 ikiwa ni miezi tisa baadaye mara baada ya kufunguliwa na kuanza kufanya kazi mwaka 2018.

Meneja mkuu wa NORECU mkoa wa Njombe Samuel Mlumba,amebainisha hayo katika mkutano na wanachama uliofanyika mjini Njombe,huku akibainisha kuwa zipo sababu mbali mbali ikiwemo changamoto za uongozi zilizosababisha kiwanda hicho kufanya kazi kwa muda mfupi na kutokana kuondoshwa kwa changamoto hizo hakuna sababu itakayozuia kiwanda hicho cha uchakataji wa Sembe kuanza kufanya kazi.

Mlumba amesema Kiwanda kilichopo mjini Njombe kilichosimama March 2019 huku kikiwa kimefanya kazi miezi 9 tangu kilipoanza kufanya kazi June 2018 kinatarajiwa kuanza uzalishaji kuanzia June mpaka March mwaka wa fedha wa 2022

“Sababu zilizopelekea kufanya kazi kwa miezi 9 safari hile sasa hivi hazipo,kwasababu zilikuwa ni changamoto za kiutumishi na usimamizi wa kiwanda hicho”alisema Mlumba

Aliongeza “Tupo kwenye mkakati wa kutafuta wataalamu waweze kututengenezea mpango biashara kwa ajili ya kiwanda cha kuchakata Sembe”aliongeza Mlumba

Nestory Betram ni kaimu mhasibu mkuu wa NJORECU,amesema kabla ya kufika mwaka wa fedha wanatarajia kununua tani za mahindi 1199.7 zenye tahamani ya shilingi milioni 600 kutoka kwenye AMCOS mbali mbali.

Benedict Mwageni ni Mwenyekiti wa bodi ya mpito wa chama kikuu cha ushirika mkoa wa Njombe,ametoa wito kwa wakulima walioko kwenye AMCOS kujiandaa kunufaika kwa kuwa kiwanda hicho kinaenda kuongeza thamani ya mazao.

“Soko la kwanza la mahindi la wana Njombe liwe ni Chama kikuu cha ushirika, kiwanda chetu kitakapoanza kufanya kazi,tunatarajia kila siku kuchakata Mahindi tani zisizokuwa pungufu ya 15 kwa hiyo kwa mwaka tutakuwa na kilo 4500”alisema Benedict Mwageni

Romanus Lugome na Mariana Chaula ni miongoni wa viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS) mkoani Njombe wameshukuru uongozi wa Chama Kikuu kuona namna ya kufufua matumaini ya muda mrefu ya Chama kundeleza miradi yao ikiwemo kiwanda hicho kitakachokuwa na msaada kwa wakulima wa Mahindi.
 Samuel Mlumba Meneja mkuu wa NORECU mkoa wa Njombe akieleza namna walivyojipanga kuendeleza miradi ya Chama ikiwemo uendeleaji wa eneo lililopo kata ya Mlangali wilayani Ludewa lililotengwa kwa dhumuni la kujenga kiwanda kingine cha kuchakata Sembe mkoani Njombe.
Baadhi ya viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS) Katika mkutano mkuu wakiwa makini kusikiliza ajenda ya fedha na mipango ya Chama kikuu ili kuimarisha ushirika mkoani humo.
Moja ya mitambo ya kiwanda cha kuchakata mahindi kinachomilikiwa na NJORECU kilichopo kata ya Njombe mjini wakati kilipoanza kufanya kazi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad