Na Chalila Kibuda, Michuzi Tv
Mkurugenzi
Msaidizi wa Mazao ya Mifugo, Usalama wa Chakula na Lishe, Bw Gabriel
Bura amewataka wakaguzi wa zao la Ngozi wa Kanda ya Mashariki kusimamia
ubora wa Ngozi zinazozalishwa.
Bura
ameyasema hayo leo (12.01.2021) wakati akifungua mafunzo ya siku mbili
ya wakaguzi wa Ngozi wa Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na
Morogoro) yanayofanyika katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es
Salaam.
Wakaguzi
hao wa Ngozi wametakiwa kusimamia uzalishaji wa zao hilo katika hatua
zake zote ili kupata Ngozi zinazofaa kusindikwa katika viwanda.
Aidha,
wakaguzi hao wametakiwa kutumia sheria namba 18 ya mwaka 2008
inayolenga kuboresha zao la ngozi ili wadau waweze kuzalisha ngozi bora
inayokidhi mahitaji ya viwanda vyetu na hatimaye kuwa na tija ya
uzalishaji wa zao hilo.
Bura
amesema uzalishaji wa ngozi za ng’ombe na mbuzi kwa siku ni vipande
31,000 lakini ni asilimia 10 tu ya ngozi zinazopelekwa viwandani hufaa
kwa ajili ya kusindikwa, na asilimia 90 hazifai kutokana na kukosa ubora
unaofaa kwa ajili ya kusindikwa.
“Hivyo
baada ya kupata mafunzo haya ni matarajio ya wizara kuwa mtakwenda
kulisimamia nyema zao hili la Ngozi ili kuhakikisha Ngozi yote
inayozalishwa inakuwa bora,” alisema Bura.
Hapa
nchini vipo viwanda viwili tu vyenye uwezo wa kusindika ngozi hadi hatu
ya mwisho ambavyo ni Moshi Leather Industry chenye uwezo wa kusindika
futi za Mraba elfu 15,000 kwa siku na Himo Tannery and Planter Ltd
chenye uwezo wa kusindika futi za mraba 10,000 kwa siku.
Uwezo
wa usindikaji wa viwanda vyote viwili kwa siku ni sawa na vipande 1000
vya ngozi ya ng’ombe na 9000 vya ngozi ya mbuzi, hivyo bado kuna uhitaji
wa viwanda vya kusindika Ngozi na vilivyopo kuongeza uwezo wake wa
kusindika zao hilo.
Kaimu
Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo,Usalama wa Chakula na Lishe wa
Wizara ya Mifugo na Uvuvi (sekta ya Mifugo) Bw.Gabriel Bura akizungumza
na wakaguzi wa Ngozi Kanda ya Mashariki wa mkutano huo uliofanyika
Jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo,Usalama wa Chakula na Lishe wa
Wizara ya Mifugo na Uvuvi (sekta ya Mifugo) Bw.Gabriel Bura akiwa katika
picha ya Pamoja na wakaguzi wa Ngozi Kanda ya Mashariki mara baada ya
kufunguliwa mkutano huo.
No comments:
Post a Comment