Pichani ni Mkurugenzi Mkuu LATRA Gilliard Ngewe (wa katikati) akiwa na Salum Pazzy ambaye ni Afisa Habari Mwandamizi LATRA (Kulia kwa Mkurugenzi Mkuu) aliyevaa suti ya bluu, pamoja na Tadei Mwita ambaye ni Meneja Mradi wa Taketi Mtandao LATRA (kushoto kwa Mkurugenzi Mkuu)
***************************
Mamlaka inawaagiza wasafirishaji wote wa abiria kwa mabasi kuzingatia masharti ya leseni za usafirishaji na matakwa ya Kanuniza Leseni za Usafirishaji -Magari ya Abiria zilizotangazwa kwa tangazo na 76 kwenye gazeti la Serikali Februari 7, 2020 kama ifuatavyo;
Kanuni ya 4(2)(c); “Leseni ya kusafirisha abiria itatolewa kwa muombaji aliyesajiliwa kwenye mfumo wa tiketi za kielektroniki ulioidhinishwa na Mamlaka”.
Kanuni ya 24(b)(d); “Msafirishaji mwenye leseni ya kusafirisha abiria wa masafa marefu ahakikishe anatoa tiketi za kielektroniki kwa abiria.”
Mamlaka inawataka wasafirishaji watoetiketi za kielektroniki kama kanuni zinavyoelekeza. Kuanzia tarehe 6Januari, 2021 hakuna msafirishaji atakayeruhusiwa kusafirisha abiria bila kutoa tiketi za kielekroniki kwa abiria wotekatika njia zifuatazo;
i. Dar-es-Salaam –Tanga
ii.Tanga –Arusha
iii. Dar es Salaam –Lindi
iv. Dar es Salaam –Mtwara
v. Dar es Salaam-Iringa
vi. Dar es Salaam –Njombe
vii. Dar es Salaam –Ruvuma
viii. Dar es Salaam –Mbeya
ix. Dar-es-Salaam-Tunduma
x. Dar es Salaam –Rukwa
xi. Dar es Salaam –Morogoro
xii. Dar es Salaam –Kilombero
xiii. Dar es Salaam –Ifakara
xiv. Dar es Salaam –Malinyi
xv. Dar es Salaam –Mahenge
No comments:
Post a Comment