Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) imeikabidhi Kampuni mpya ya Afcons mara baada ya kuvunja
mkataba wa Mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Chalinze kutoka Kampuni ya
OIA ya India kwa kushindwa kukabidhi mradi kwa wakati.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Dawasa Cpyprian Luhemeja ameyasema hayo leo alipofanya
ziara ya ukaguzi wa miradi ya maji pamoja na kuzungumza na wafanyakazi
wa Dawasa Chalinze na Wami.
Alisema
kuwa kwa sasa mradi wa Chalinze awamu ya tatu umepata majibu kwani
tayari amepatikana mkandarasi mpya kutoka Kampuni ya Afcons ambaye
amepewa miezi nane kukamilisha mradi huo.
Alielezea
kuwa mkandarasi huyo alikuwa akiwasumbua kwa muda mrefu kwa kufanya
kazi chini ya kiwango na kusababisha wananchi wa Chalinze kukosa huduma
ya maji kwa muda mrefu kwani alitakiwa kukamilisha mradi huo mwaka 2017
lakini pamoja na kuongezewa muda alishindwa kukamilisha.
Alimtaka
mkandarasi huyo mpya kutoka Kampuni ya Afcons kuhakikisha anatekeleza
mradi huo kwa wakati kwani akienda tofauti na makubaliano ya mkataba
hatosita kumfukuza kwani wananchi wamechoka kusubiri na kuteseka kwa
kukosa huduma ya maji.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Dawasa Cpyprian Luhemeja akitoa maelekezo kuhusu
mitambo ya kusukumia maji iliyoletwa na mkandarasi mpya ya Afcons baada
ya kusitisha mkataba wa Mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Chalinze kutoka
Kampuni ya OIA ya India kwa kushindwa kukabidhi mradi kwa wakati.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Dawasa Cpyprian Luhemeja akizungumza na waandishi wa
habari kuhusu Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam
(DAWASA) ilivyovunja mkataba wa Mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Chalinze
kutoka Kampuni ya OIA ya India kwa kushindwa kukabidhi mradi kwa wakati
na kumpatia mkandarasi mpya ambayo ni kampuni ya Afcons.
No comments:
Post a Comment