Taasisi tatu za ukopeshaji wa fedha wilayani Tunduru zimemtapeli Mwalimu Mstaafu Kanyinga Abdallah zaidi ya shilingi milioni 50.
Mwalimu
huyo alikopa jumla ya shilingi milioni 10,350,000/- kwenye taasisi tatu
tofauti za ukopeshaji fedha wilayani Tunduru, lakini ndani ya mwaka
mmoja alipopata pensheni yake taasisi hizo zikampora jumla ya shilingi
milioni 59 ikiwemo pesa walizomkopesha na riba ya wastani wa asilimia
600 hadi 1,000.
Akizungumza na vyombo vya habari mjini Tunduru
Jumapili ya leo, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro amemkabidhi
mzee huyo ambaye ni mwalimu mstaafu, kiasi cha shilingi milioni 7 ambazo
zimerejeshwa na taasisi hizo ambazo zinapaswa kurejesha kiasi
kilichobaki cha shilingi milioni 52 ifikapo mwishoni mwa mwezi Januari
2020.
Mtatiro amempongeza sana Kamanda wa TAKUKURU wilayani
Tunduru kwa kutekeleza maagizo yake ya kuhakikisha kila mwananchi
aliyewahi kuibiwa na taasisi za utoaji mikopo, na ana ushahidi, aweze
kurejeshewa fedha zake na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.
Akizungumza
kwa bashasha na kulengwalengwa na machozi Mzee Kanyinga Abdallah
ameeleza haamini anachokiona "...niliamini kuwa sitazipata pesa zangu
kwa sababu wakopeshaji hawa wana nguvu na wana mtandao mkubwa.
Namshukuru sana DC wetu wa Tunduru na Kamanda wa TAKUKURU kwa msaada
wao...Mungu atawalipia".
Mwezi Aprili 2020, Mtatiro alitoa
maelekezo kwa taasisi za utoaji mikopo, kuachana na biashara ya
kuwadhulumu wananchi kwenye wilaya yake, na aliielekeza TAKUKURU
kuchukua hatua kali sana.
No comments:
Post a Comment