Katibu wa Machinga Network mkoa wa Iringa Joseph Kilienyi akizungumza na wafanyabiashara wadogo wadogo wakati akieleza kuridhishwa kwa mwenendo wa biashara kwa wafanyabiasha hao wa soko la mashine tatu manispaa ya Iringa.
Na Fredy Mgunda,Iringa.
Wafanyabiashara wadogo wadogo wa mkoa wa
Iringa(MACHINGA NETWORK)wameridhishwa na hali ya kibiashara inavyoendelea hivi
sasa baada ya mlipuko wa ugonjwa wa Corona ambao ulisababisha hasara kwa
wafanyabiashara hao.
Wakizungumza na blog hii
wafanyabiashara wa soko la mashine tatu walisema kuwa biashara zimerejea
katika hali ya kawaida kama ilivyokuwa awali na wameanza kupata faida na
kurudisha mitaji yao iliyokuwa imeyumba kipindi cha ugonjwa wa Corona.
Antony mashaka alieleza kuwa kipindi
cha Corona alikuwa anashindwa kuuza biashara yake ya mitumba katika soko hilo
kwa wingi kutokana na mashariti yaliyokuwa yamewekwa kutokana na uwepo wa
ugonjwa wa Corona lakini kwa sasa anauza kwa faida kwa kuwa hakuna yale mashariti
tena.
"Ndugu mwandishi angalia hapa
kuna wateja wengi ambao wanachagua nguo za mitumba bila mashariti kama
ilivyokuwa kipindi cha Corona ndio maana saizi tunasema biashara imerudi kama
ilivyokuwa awali kabla ya Corona na faida tunapata kubwa ndio maana tupo
hapa"alisema Mashaka
Mashaka aliongeza kwa kuwaomba wateja
wa nguo za mitumba kwenda katika soko hilo kununua nguo hizo zinazouzwa kwa bei
nafuu na wasiogope msongamano mkubwa kwa kuwa saizi hakuna tena ugonjwa wa
Corona kama ambavyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe
Magufuli ambavyo amekuwa akisisitiza kuwa hakuna tena ugonjwa huo hapa nchini
Bi Amina Salum ambaye ni
mfanyabiashara wa viazi mviringo alisema kuwa ulikuwa wakati mgumu sana kufanya
biashara kipindi cha Corona kutokana na hofu iliyokuwa imetanda kwa miongoni
mwa watanzania na dunia kwa ujumla juu ya ugonjwa huo ambao ulikuwa tishio
kubwa kwa dunia na bado tishio kwa baadhi ya nchi ambazo bado ugonjwa huo
upo.
"Kwa kweli tunamshukuru Mungu
kwa kutuepusha na Corona kwa sababu saizi tunafanya kazi zetu za kibiashara
kama mwanzo na wateja wanakuja kununua bidhaa zetu bila ya kuwa na hofu yoyote
ile ya ugonjwa huo" alisema Salum
Nao baadhi ya wanunuzi katika soko la
mashine tatu walisema kuwa walikuwa wanahofu kubwa ya kwenda sokoni hasa katika
soko hilo kutokana na mashariti yaliyokuwepo kipindi cha ugonjwa wa Corona
hivyo kusababisha kushindwa kufika katika soko hilo.
Lakini walieleza kwamba baada ya
ugonjwa wa Corona sasa wanaendelea kwenda kupata huduma kwenye soko hilo ambalo
bidhaa zake zinapatikana kwa bei nafuu kuliko maeneo mengine na kuongeza
mzunguko wa biashara katika soko hilo.
"Saizi tunakuja sokoni bila
shaka yoyote ile kununua bidhaa zetu tunazozitaka kutokana na mahitaji yetu
ambayo tunahitaji katika soko hilo la mashine tatu"walisema
Kwa upande wake katibu wa Machinga
Network mkoa wa Iringa Joseph Kilienyi alisema kuwa baada ya ugonjwa wa Corona
biashara zimerejea katika hali ya kawaida na wafanyabiashara wadogo wadogo
wanaendelea kufanya biashara kama kawaida.
"Ukiangalia saizi maeneo yote ya
kibiashara yanaendelea na biashara kama kawaida kutokana na kuondolewa na
mashariti ya ugonjwa wa Corona hivyo wafanyabiashara na wanunuzi wapo
huru" alisema kilenyi
No comments:
Post a Comment