Pichani Ni Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania Bwana Imani Sichalwe akiwa na viongozi wa Umoja wa wabeba Nyama Kwenye bodaboda Machinjio ya Vingunguti.
Na.Vero Ignatus.
Bodi
ya nyama nchini imejipanga kuandaa utaratibu mzuri wa usajili wa
wabeba nyama kwa njia ya pikipiki(bodaboda), kutoka katika machinjio
hadi kwenye mabucha mbalimbali ya nyama Nchini.
Hayo yamesemwa na Kaimu msajili wa bodi ya nyama nchini Imani Sichalwe,
wakati akizungumza na Viongozi wa Umoja wa wasafirishaji wa nyama kwa
kutumia pikipiki (bodaboda), wanaofanya shughuli zao kwenye machinjio ya
vingunguti Dar-es-Salaam.
Sichalwe
amesema kuwa kwa mujibu wa taratibu na sheria, hairuhusiwi kufanya
biashara ya nyama, kama haujasajiliwa na bodi ya nyama,na katika
usajili huo bodi ya nyama imekuwa ikisajili magari ya kubebea nyama ,ila
wabebaji wa nyama kwa njia ya pikipiki yaani bodaboda ndio waliokuwa
hawajasajiliwa ,licha ya kuonekana wakisafirisha nyama.
Amesema
kwa mujibu wa kanuni zilizopo za usajili na ukaguzi , zinayohusu
biashara ya nyama hairuhusiwi kusafirisha nyama kwa njia ya bodaboda,Kwa
Muktadha huo bodi ya nyama ikaona ni vyema kuja na mpango wa
kuwasajili, ili waweze kutambulika na kupewa utaratibu mzuri,wa kubeba
nyama kwasababu nyama ni kitoweo muhimu sana kwa binadamu na ndio Maana
zikawepo kanuni mbalimbali,Miongozo na sheria lengo likiwa ni kuongeza
ubora na usalama wa nyama Nchini.
Sichalwe
amesema kiutaratibu nyama hairuhusi kubebwa kwenye Vifaa vyovyote vya
plastiki, isipokuwa kwenye vyombo vya alminiamu ,au vile vyombo ambavyo
ni rahisi kusafishika na havitoi kutu,kwa hivyo utaratibu unaotumika
kubeba nyama kwenye bodaboda ni kinyume na utaratibu.
''Kwakuwa
hutumika mifuko ya salfeti kuwekea nyama na utakuta mifuko yenyewe ni
michafu, kisha wanatumbukiza nyama kwenye madeli ya plastiki ,ambayo sio
rahisi kusafishika jambo linaloharibu ubora na na kuhatarisha usalama
wa mtumiaji''Alisema Sichalwe.
Aidha
miongoni mwa majukumu ya bodi ya nyama nchini ni Kuendeleza sekta ya
nyama, hivyo bodi hiyo imeona ni vyema kutumia utaratibu wa kukutana na
viongozi wa umoja wa wabeba nyama ,kwa bodaboda machinjio ya vingunguti
na kuwapa elimu,Pamoja na kuwaelezea juu ya uwepo wa fursa za ufanyaji
wa biashara ya kusafirisha nyama kwa bodaboda, kwa mujibu wa sheria na
kanuni na miongozo inayohusiana na utaratibu mzuri wa ubebaji nyama kama
sheria na kanuni, zinavyoelekeza ili kuendeleza falsafa ya bodi isemayo
nyama bora na salama kwa wote.
Akiongelea kifaa hicho maalumu ambacho kitakuwa kinatumika kubebea nyama,kitakachokuwa kinafungwa kwenye bodaboda Imani Sichalwe ,amesema
kitakuwa hakiwezi kuruhusu joto wala baridi kuingia isipokuwa ukiweka
nyama joto ambalo lipo mule ndani ya hicho kifaa maalumu, linabaki vile
vile hivyo, kinachotakiwa
hapo ni kuweka barafu kwasababu nyama inatakiwa iwe kwenye ubaridi
kisha unafunga ,hivyo kufanya nyama iendelee kuwa safi na salama tofauti
na wanavyosafirisha sasa.
''Mvua
ikinyesha inanyeshea nyama,wakipita kwenye maji machafu
yanamwagikia,wakipita kwenye vumbi linaingia kwenye nyama jambo ambalo
linasababisha nyama kupoteza ubora na kuhatarisha afya ya mlaji''Alisema
Akizungumza kwa niaba ya wenzake Mwenyekiti wa Umoja wa wabeba nyama kwa bodaboda machinjio ya vingunguti Godfrey Jastini ,ameshukuru
hatua ya bodi kuja na mkakati wa kuwatambua kwa mujibu wa sheria ,na
kuwasajili ili wabebe nyama kwa utaratibu mzuri jambo litakalopelekea
kuongeza usalama wa nyama kwa mtumiaji ,na kuomba mpango huu ufanye
haraka ili vijana waweze kufanya biashara ,hii kwa uhuru na kufuata
sheria na kanuni za usafirishaji wa nyama Nchini.
‘’Nitakwenda
kufanya kikao na wanachama wangu kuwaeleza juu bodi ya nyama nchini,na
ni ukweli usiopingika vijana wengi tumehamasika kufanya biashara hii ya
ubebaji wa nyama kwa njia ya bodaboda kutoka kwenye machinjio japo
tunakutana na vikwazo vingi kwasababu hatujasajiliwa kwa mujibu wa
sheria, na hata ubebaji baadhi yetu hatuzingatii usafi na
usalama, ukizingatia vyombo tunavyobebea sio salama kwakuwa
havisafishiki kwa urahisi,kwa hiyo tunashukuru sana kwa Elimu nzuri ya
namna bora ya ubebaji wa nyama kwenye bodaboda na kuambiwa uwepo wa
vifaa maalumu vya kubebea nyama kwenye bodaboda kutoka kwenye machinjio
hadi kwa mabucha ya kuuzia nyama’’alisema Godfrey Jastini Mwenyekiti
wa umoja wa wabeba nyama kwenye bodaboda machinjio ya Vingunguti.
Mpango
huu wa usajili wa madereva wa bodaboda wanaobeba nyama ,kutoka kwenye
machinjio mbalimbali kwenda kwenye mabucha, utafanyika nchi nzima na
utasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza wigo kwa vijana kujiajiri, katika
ubebaji wa nyama kwenye bodaboda, ikiwa na utekelezaji wa kauli mbiu ya
bodi ya nyam,a inayosema ‘’Nyama bora na salama kwa wote’’ Jambo
litakalosaidia kuchochea kasi ya maendeleo ya sekta ya nyama Nchini.
No comments:
Post a Comment