Mwenyekiti
wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga,
Dk. Rose Malisa ambaye ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa
Shinyanga akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga. Wa kwanza kushoto ni Katibu wa
Chama Cha Wafanyakazi (TUGHE) mkoa wa Shinyanga, Gaudensi Kadyango
akifuatiwa na Kaimu Mwenyekiti wa TUGHE mkoa wa Shinyanga, Rajabu
Masanche akifuatiwa na Mwakilishi wa Mganga Mkuu mkoa wa Shinyanga,
Timoth Sosoma.
Mwenyekiti
wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga,
Dk. Rose Malisa ambaye ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa
Shinyanga akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mwakilishi
wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Timoth Sosoma akizungumza wakati
akizindua Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Shinyanga.
Mwakilishi
wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Timoth Sosoma akizungumza wakati
akizindua Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Shinyanga.
Katibu
wa Chama Cha Wafanyakazi (TUGHE) mkoa wa Shinyanga, Gaudensi Kadyango
akitoa mada ya wajibu na majukumu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga na umuhimu wa Chama cha
Wafanyakazi.
Kulia
ni Katibu Msaidizi wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa ya
mkoa wa Shinyanga Allan Luvanda akifuatiwa na Katibu wa Baraza hilo,
Clementina Salutari na Mwenyekiti wa Baraza hilo Dk. Rose Malisa. Wa
kwanza kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa TUGHE mkoa wa Shinyanga, Rajabu
Masanche.
Wajumbe
wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga
wakipiga picha ya pamoja baada ya Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Na Kadama Malunde
Mwakilishi
wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Timoth Sosoma amezindua rasmi
Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga ambalo
litakuwa na jukumu la kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha na
kuboresha utendaji na uwajibikaji ndani ya hospitali utakaowezesha
hospitali kutoa huduma kwa wananchi kwa haraka,uwazi,urahisi,gharama
nafuu wakati wowote.
Uzinduzi
huo umefanyika leo Jumatano Novemba 4,2020 katika Hospitali ya Rufaa ya
Mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga pamoja na viongozi wa Chama Cha
Wafanyakazi (TUGHE) mkoa wa Shinyanga.
Akizindua
Baraza hilo la Wafanyakazi, Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga, Timoth Sosoma amesema baraza hilo litakuwa chachu ya
kuboresha huduma za afya katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga
huku akiwasisitiza wajumbe kuwa waadilifu na kuzingatia maadili ya
utumishi wa umma.
“Hiki
ni kikao cha kwanza cha Baraza la Wafanyakazi tangu mabadiliko ya kuwa
chini ya Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto.
Mkiwa sehemu ya historia hii ni matumaini yangu kuwa nafasi mliyopewa
mtaitumia vizuri kwa ajili ya kushauri namna bora ya kuboresha utendaji
kazi na kujenga mahusiano baina ya Mwajiri na Mwajiriwa”,amesema Sosoma.
“Madhumuni
ya kuundwa kwa mabaraza ya wafanyakazi ni kuishauri serikali kuhusu
usimamizi wa kazi na rasilimali,utekelezaji wa majukumu,kulinda haki na
wajibu wa Waajiri na Wafanyakazi,kutoa ushauri kuhusu kujenga hali bora
za kazi na maslahi na kusimamia haki na ustawi katika sehemu za
kazi”,ameongeza Sosoma.
Amesema
Baraza la Wafanyakazi kama vyombo vya ushauri na usimamizi yana wajibu
wa kuhakikisha kuwa waajiri na watumishi wanatambua wajibu na haki zao
na wanazingatia maadili ya utumishi wao kuleta mabadiliko ya utendaji
kazi yenye tija, staha na upendo.
“Maadili
ni kitu muhimu cha kuzingatia katika utendaji kazi. Ni lazima kila
mtumishi wa umma kujiepusha na vitendo vinavyoashiria ukosefu wa maadili
kama vile rushwa,utovu wa nidhamu,utoaji wa siri za serikali na huduma
mbaya kwa wagonjwa”,amesisitiza Sosoma.
Aidha
amewataka wajumbe wa Baraza hilo kufanya vikao walau mara mbili kwa
mwaka kwa mujibu wa sheria ili kuepusha fursa kwa wafanyakazi kukuza
majungu mahala pa kazi na kwamba vikao hivyo havipaswi kupuuzwa hivyo
viandaliwe katika viwango vinavyokidhi malengo na makusudio ya sheria.
Naye
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa
Shinyanga, Dk. Rose Malisa amewaomba wajumbe wa baraza hilo kuzingatia
majukumu yao ambayo ni pamoja na kuwashirikisha wafanyakazi wa serikali
katika utekelezaji wa shughuli za hospitali kwa ushirikiano na uongozi
wa hospitali na kuishauri Menejimenti juu ya ufanisi wa kazi na hatua
zinazofaa kuchukuliwa kuboresha huduma za afya na maslahi ya
wafanyakazi.
Aidha
Dk. Malisa ambaye ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa
Shinyanga amewataka wajumbe wa baraza hilo kuwa chachu ya mabadiliko
katika kuboresha huduma za afya katika hospitali na kuendelea kutoa
elimu ya afya kwa jamii.
Kwa
upande wake, Katibu wa Chama Cha Wafanyakazi (TUGHE) mkoa wa Shinyanga,
Gaudensi Kadyango amewataka wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kufanya kazi kwa bidii,kujipenda
na kuwa mfano bora kwa watumishi wengine wa umma.
Aidha
amewakumbusha watumishi wa umma kuzingatia maadili ya kazi yao ikiwa ni
pamoja na kuepuka kutumia lugha mbaya kwa wateja na kuendekeza matumizi
ya simu za mkononi wakati wa kazi.
Uzinduzi
wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Rufaa mkoa wa Shinyanga
umekwenda sanjari na uchaguzi wa viongozi Baraza hilo ambapo
Clementina Salutari amechaguliwa kuwa Katibu na Allan Luvanda kuwa
Katibu Msaidizi.
No comments:
Post a Comment