Mkurugenzi
Msaidizi kitengo cha Magonjwa yasiyo ambukiza,Wizara ya Afya Dkt. James
Kaologwe akizungumza na wadau wa macho wakati wa uzinduzi wa mradi wa
boresha macho uliofanyika kwenye hotel ya Nashera jijini Dodoma
Mkurugenzi
wa Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Ofisi ya Rais-Tamisemi Dkt.
Ntuli Kapologwe akiongea wakati wa ufunguzi wa Mradi wa boresha macho
ulio chini ya Shirika lisilo la kiserikali la SightSavers.
Picha ya pamoja ya wadau wa macho mara baada ya uzinduzi wa mradi wa boresha macho
Baadhi
ya washiriki wa uzinduzi huo ambapo mradi huo una thamani ya shilingi
bilioni sita za kitanzania na utakua katika mikoa mitanoMeneja Mipango na Mshauri Mwelekezi wa Shirika la Sight Savers Mhandisi Koronel Kema akizungumza kuhusu mradi huo mpya.
************************************
Na.WAMJW-Dodoma.
SERIKALI
imesema haitasita kumchukulia hatua Mganga Mkuu wa Mkoa au Wilaya
atakayebainika kushindwa kusimamia fedha za Mradi wa Boresha Macho.
Kauli
hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa
Jamii, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi)
Dkt.Ntuli Kapologwe leo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Boresha Macho
unaotekelezwa na Shirika lisilo la kiserikali la Sightsavers kwa
ufadhili wa Shirika la Misaada la Uingereza(UKAID).
Dkt.Kapologwe
amesema mradi huo unagharimu Shilingi za kitanzania Bilioni 6 “lazima
kuwepo na usimamizi mkubwa wa fedha hizo ili kufikia malengo
yaliyokusudiwa”.
Ameendelea
kusisitiza kuwa kama kuna Mganga mkuu ambaye atashindwa kusimamia
vizuri fedha za mradi huo atajieleza kwanini hawezi kusimamia.
“Tuchukue
mradi huu kama mtoto wetu na malengo tuliyoweka lazima
yafanikiwe,hatutamvumilia mtu yeyote aidha anatoka shirika lisilo la
kiserikali au serikalini ambaye hatatekeleza inavyotakiwa, kwasababi
hizi fedha zimeletwa kwa ajili ya watanzania na wanapaswa kunufaika na
kila uwekezaji unaofanywa kwenye macho,”Amesema Dkt.Kapologwe.
Aidha,
Dkt. Kapologwe ameeleza kuwa suala la ubora wa kazi itakayofanyika ni
la msingi ili mradi ufanyike kwa malengo yaliyokusudiwa huku akisema
pale itakapobainika mradi hautekelezwi ipasavyo serikali haitasita
kuchukua hatua.
“Kila
senti moja ambayo imetolewa kwa ajili ya mradi huu lazima iwafikie
walengwa ambao ni wananchi, sisi Tamisemi na Wizara ya Afya tutafanya
ufuatiliaji wa karibu ili kuona kama kuna thamani ya fedha kwenye
utekelezaji wa mradi huu, Sh.Bilioni sita za mradi tunataka tuone
vitu,”Amesema.
Hata hivyo amesema serikali imekuwa ikiendelea kuimarisha huduma za afya kwa wananchi ambapo zimeshuka hadi ngazi za kijiji.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Wizara ya Afya anayeshughulia
magonjwa yasiyo ambukiza, Dkt.James Kiologwe, amesema asilimia moja ya
watanzania wanakabiliwa na tatizo la uoni ambao unasababisha kupata
upofu.
Hata
hivyo, amesema asilimia 75 ya matatizo yanayosababisha upofu
yanazuilika na Wizara ya Afya inajivunia kufanya kazi na wadau
kuhakikisha idadi hiyo ya watu wanapata tiba ili wasipate upofu.
“Katika
ushirikiano huo kuna mambo tunajivunia hadi sasa, tumeweza kuratibu
vizuri wadau, tunajua katika viwango vya kimataifa tunatakiwa kuwa na
hospitali moja ya kutoa huduma za upasuaji kwa watoto wanaopata matatizo
ya macho, tunafurahi hadi sasa kuna hospitali nne ambazo zinauwezo
huo,”.
Awali,
Meneja Mipango na Mshauri Mwelekezi wa sightsaves Eng. Koronel Kema,
amesema mradi huo utagharimu kiasi cha Sh.Bilioni sita na unatarajiwa
kupima na kutoa huduma za macho kwa watu 150,000 huku kati yao 13,500
watakaobainika na mtoto wa jicho watafanyiwa upasuaji.
Aidha, amesema mradi huo pia utaongeza uelewa kwa watu 650,000 kuhusu umuhimu wa kupata huduma za macho.
“Mradi
utafikia halmashauri tano kati ya tisa za Mkoa wa Morogoro na kwa Mkoa
wa Singida Halmashauri zote tisa zitanufaika,”amesema.
No comments:
Post a Comment