

Uzinduzi
 wa Kampeni uliofanyika hapo jana Septemba 13 katika kitongoji cha 
Mdaula Chalinze uliweza kuongozwa na mgeni rasmi ambae ni Mgombea nafasi
 ya Ubunge kupitia chama cha Mapinduzi CCM, Ridhiwani Kikwete,ambae 
aliweza kunadi sera zake kwa kuhakikisha jimbo la Chalinze linabaki 
mikononi mwake kwa kuhitaji wananchi wamachagua yeye ili aweze 
kuendeleza maendeleo katika Jimbo hilo. 

Mbali
 na hapo alipanda aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Ulanga katika Mkoa wa 
Morogoro ndugu Goodluck Mlinga na kutema cheche zake za kuhakikisha 
anaunga mkono juhudi za chama chake cha mapinduzi nchi nzima kinapata 
ushindi kuanzia Madiwani, Wabunge mpaka  Mh. Dkt John Pombe Magufuli kwa
 kupata ushindi mkubwa Katika kinyang'anyiro cha kiti cha urais, hali ya
 kuwa ndugu Mlinga amepoteza nafasi ya kugombania ubunge kwa awamu hii.




No comments:
Post a Comment