Na Said Mwishehe, Michuzi TV –Simiyu
MGOMBEA
Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) ambaye pia ni Rais wa
Tanzania Dk.John Magufuli amesema ili kuwa na uchumi imara katika nchi
lazima uanze na vitu vinavyochochea uchumi.
Dk.Magufuli
amesema hayo leo mbele ya maelfu ya wananchi wa Mkoa wa Simiyu
alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni za kuomba kura kuelekea uchaguzi
mkuu unaotatarajia kufanyika Oktoba 28 mwaka huu.
Amesema
katika nchi yoyote ukitaka kujenga uchumi ni lazima uanze na vitu
vinavyochochea uchumi, huwezi kutaka kujenga uchumi wakati vitu
vinavyochochea uchumi havijaendelezwa,
“Hata
Mungu mwenye alipotaka kuiumba Dunia hakuanza na watu, alianza na ardh
ili watu waje waitumie kulima,akaleta jua ,a akaleta dunia baadae
akaleta wanyama na ndege ili binadamu watakapokwenda katika ardhi ile
wakaiwatawale na alitumia siku sita na ya saba akampumzika,”amesema
Dk.Magufuli
Hata
hivyo amefafanua mbele ya wananchi wa Mkoa wa Simiyu kwamba alipoingia
madarakani aliona atumie mbinu ya kujenga uchumi wa kisasa katika nchi
hii na ndio maana walianza na miundombinu na anakumbuka hata Bariadi
watu walikuwa wanakufa bila kutibiwa hospitali na walikuwa wanabebwa
kwenye tela za ng’ombe.
“Mmesahau,
tukasema lazima tujenge hospitali kubwa ya Rufaa itakayofanya upasuaji
wa aina zote, wakati nakwenda kuweka jiwe la msingi watu hawakuwamini
kama kutakuwa na hospitali ya rufaa , leo pale Itilima, leo haa Bariadi
hospitali ipo,
Wakati
anaingia madarakani hii barabara haikuwepo na anakumbuka wakati
anabomoa nyumba zilizokuwepo kwenye hifadhi ya barabara alisema ipo siku
moja watu wa Simiyu watafurahi.”Tumejenga miundombinu ya barabara ili
kutengeneza uchumi wa kisasa”.
Akizungumza
zaidi na wananchi wa Simiyu amewaahidi kwamba wakimchagua tena miaka
mitano mingine atahakikisha ndani ya miaka mitatu vijiji vyote kijiji
kitakuwa na umeme kwani tayari vijiji zaidi ya 10,000 tayari vina umeme
na vibaki vijiji 2600.
“Nataka
kusema hili Simiyu, sitaki kusema mbele ya Mungu, mkitupa miaka mingine
mitano nina uhakika kama mitatu vijiji vyote vitakuwa na pa umeme, ndio
maana nakuja kuwaomba kwanini watu wafanye majaribio hatawatufikisha
mahali.
“Tumehangaika
wote, tumebana mafisadi wote, tumeanza viruzi, ndio maana nafikiri watu
wa Bariadi na Simiyu mnipe kura ili tuendelee,”amesema Dk.Magufuli
wakati anazungumza na wananchi hao.
MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) ambaye pia ni Rais wa Tanzania Dk.John Magufuli
No comments:
Post a Comment