Wananchi wa kata ya Ikongosi wanategea kupata maendeleo makubwa kwa miaka mitano ijayo kutokana na mikakati aliyokuwanayo mgombea udiwani wa kata ya Ikongosi Negro Sanga wakati akiomba kura za Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa kuwa yeye ameshapita bila kupigwa.
Hayo yalisemwa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mtili kilichopo kata ya Ikongosi kwa kutoa ahadi ya kukamilish ujenzi wa ofisi ya kata kwa kuwa kila kitu kipo kwenye mipango dhabiti kwa lengo la kuleta maendeleo kwa wananchi wa kata hiyo.
Sanga alisema kuwa wanatarajia kuwa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi itajengwa katika kata ya Ikongosi kwa kuwa mchakato wote ulishafanyika kwenye baraza la madiwani lilolopita hivyo wananchi wanatakiwa kuchangamkia fursa zitakazo jitokeza hapo baadae.
Alisema kwa miaka mitano iliyopita maendeleo mengi na makubwa yamefanyika katika kata hiyo kwenye sekta ya afya,miundombinu kama barabara,majengo,sekta ya michezo,elimu,kilimo na biashara hivyo wananchi wametakiwa kuendelea kukiamini chama cha mapinduzi kwa utekeleza wa Ilani yake.
“Miaka mitano mliyonipa ridhaa ya kuwa diwani wenu kwa ushirikiano mkubwa tumefanya kazi kubwa ya kujenga Ofisi za vijiji kwenye vijiji vyote vitano tena kwa ubora mkubwa na sasa kwa pamoja tunatekeleza ujenzi wa ofisi ya kata” alisema Sanga
Aidha Sanga alimuomba mgombea ubunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Exaud Kigahe kutengeneza ushirikiano ulitukuka kwa wabunge zenzake wa wilaya ya Mufindi kwa lengo la kusaidiana kuleta maendeleo kwenye wilaya ya Mufindi ambavyo inautajili mkubwa.
Mgombea udiwani huyo alimalizia kwa kumshukuru mbunge aliyemaliza muda wake Mahmoud Mgimwa kwa ushirikiano wa kimaendeleo alioutoa kwenye kata hiyo kwa kipindi chote alichokuwa madarakani kwenye jimbo la Mufindi Kaskazini.
No comments:
Post a Comment