Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo (Bara) Bw.Gerald Kusaya akiongea na
watendaji wa mradi wa Kuimarisha Uzalishaji Mpunga (ERPP) alipokagua
skimu ya umwagiliaji ya Mtwango wilaya ya Magharibi ‘B’ Zanzibar
leo.Kulia kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo( Zanzibar) Bi.Maryam
Abdulla.Katibu
Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya akizungumza na waandishi wa
habari mjini kuhusu miradi inayotekelezwa na wizara yake kwa ushirikiano
na Wizara ya Kilimo Zanzibar ikiwemo ya Kudhibiti Sumukuvu (TANIPAC) na
Kuongeza Tija na uzalishaji zao la Mpunga (ERPP)
Katibu
Mkuu Wizara ya Kilimo (Bara) Bw.Gerald Kusaya akikagua skimu ya
umwagiliaji ya Mtwango wilaya ya Magharibi ‘B’ Zanzibar inayotekelezwa
chini ya Mradi wa ERPP.
Katibu
Mkuu Wizara ya Kilimo ( Bara) Bw. Gerald Kusaya akionyesha kungua za
gari wakati alipokabidhi gari hilo pamoja na pikipiki mbili kwa Katibu
Mkuu Wizara ya Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Zanzibar Bi.Maryam
Abdulla ( kulia) leo mjini Zanzibar.Gari hilo limetolewa kwa ajili ya
uratibu wa Mradi wa Kudhibiti Sumukuvu upande wa Zanzibar.
Katibu
Mkuu Kilimo ( Bara) Bw.Gerald Kusaya aliyevaa tai akiwa na Katibu Mkuu
Kilimo (Zanzibar) Bi.Maryam Abdulla alivaa ushungi mwekundu wakiongea na
wakulima wa zao la mpunga katika skimu ya Mtwango wilaya ya Magharibi
‘B’ Zanzibar .Katibu Mkuu huyo yuko ziarani Zanzibar kukagua miradi ya
kilimo inayotekelezwa kwa pamoja na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
leo
Mratibu
wa Mradi wa Kudhibiti Sumukuvu nchini (TANIPAC) Clepin Josephat akitoa
maelezo kwa Makatibu Wakuu wizara za Kilimo Bw.Gerald Kusaya ( aliyevaa
tai) na Bi.Maryam Abdulla ( aliyevaa ushingi mwekundu) kuhusu eneo
patakapojengwa ghala la kuhifadhia nafaka tani 1,500 katika eneo la
Kizimbani Wilaya ya Magharibi ‘A’ Zanzibar leo.
No comments:
Post a Comment