Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. George Simbachawene (MB) amesema Jeshi la Polisi
nchini limefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza matukio ya uhalifu ikiwa ni
pamoja na kuziba mianya ya uingizaji na usambazaji wa dawa za kulevya,
usafirishaji wa binadamu na uhalifu unaovuka mipaka.
Waziri
Simbachawene amesema hayo leo jijini Dodoma, wakati akifunga kikao kazi cha
Maafisa Wakuu Makao Makuu, Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi
kilichofanyika kwa muda wa siku tatu, kikao ambacho kililenga kufanya tathimini
ya utendaji wa kazi za Jeshi hilo.
Kwa
upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amesema kuwa, Vyombo
vya ulinzi na usalama vimejipanga imara kuhakikisha vinaimarisha hali ya
usalama hususani kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu huku akiwataka
wananchi pamoja na wanasiasa kutimiza wajibu wao kwa kutojiingiza kwenye
vitendo vya uvunjifu wa amani.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. George Simbachawene (MB)
No comments:
Post a Comment