Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida katika ziara yake ya kikazi, mkoani Singida.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Bw.Rashid Mandoa akijibu hoja za watumishi wakati wa kikao kati ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na watumishi wa halmashauri hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri mkoani Singida.
Baadhi ya watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) katika ziara yake ya kikazi mkoanI Singida.
Mlinzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Bw.Joseph Ghaba akiwasilisha malalamiko yake wakati wa kikao kati ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na watumishi wa halmashauri hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri mkoani Singida.
Na Happiness Shayo, Singida
Watumishi wa Umma nchini wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa
ili kufanikisha juhudi za Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe.
Dkt. John Pombe Magufuli za kukuza uchumi.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) alipokuwa
akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida katika
ziara ya kikazi mkoani Singida.
Dkt. Mwanjelwa amesema kuwa ni lazima watumishi wa umma waheshimu
kazi na wahakikishe wanatimiza majukumu yao kwa kuzingatia sheria,
kanuni, taratibu na miongozo iliyopo kwa kuwa Serikali ya Awamu ya tano
haitovumilia watumishi wazembe.
“Mtumishi wa Umma ni tunu kwa hiyo ni bora ukachezea mshahara kuliko
kuchezea kazi kwa sababu wapo wanaotamani kuingia serikalini lakini
hawana fursa hiyo” Dkt. Mwanjelwa amesisitiza.
Dkt. Mwanjelwa ametoa wito kwa Watumishi wa Umma nchini kufanya kazi
kwa kuendana na spidi ya Mheshimishimi Rais, Dkt. John Pombe Magufuli
na si kwa kulegalega.
Dkt. Mwanjelwa ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ni ya
uadilifu, utendaji kazi uliotukuka , haki na haiko tayari kumuonea mtumishi
yeyote.
Aidha, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amewataka Watumishi wa Umma kuwa na
subira katika kipindi ambacho serikali inafanyia kazi changamoto zao za
malimbikizo ya mishahara, kupandishwa madaraja na nyinginezo.
Mhe.Dkt. Mwanjelwa yupo katika ziara ya kikazi Mkoani Singida kwa lengo
la kukagua utekelezaji wa shughuli za TASAF na kukutana na Watumishi
kwa lengo la kusikiliza maoni na kutatua kero zao.
No comments:
Post a Comment