HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, January 21, 2020

HER INITIATIVE YARATIBU UENDESHAJI WA MRADI WA PANDA 2020, WENYE LENGO LA KUWAWEZESHA WASICHANA KIUCHUMI

Timu ya taasisi ya Her Initiative wakifurahi pamoja wakati wakiwa katika maandalizi ya mafunzo  ya ujasiriamali kupitia mradi wa Panda kwa mwaka 2020, yatakayofanyika hivi karibuni jijini Dar es salaam. Zaidi ya wasichana 30 kutoka sehemu mbalimbali watashiriki katika mafunzo ya uundaji na utoaji huduma katika jamii zao ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Sehemu ya Majaji katika mafunzo ya ujasiriamali kupitia mradi wa Panda kwa mwaka 2020 ambao pia ni washirika (partners) wakimfamfia usaili mmoja wa wasichana watakaoshiriki mafunzo hayo katika kipengele cha mradi (Mapambo, Uokaji keki na mapishi).

Na  Diana Aggrey. 

Kwa mara nyingine , taasisi ya Her Initiative  imeratibu uendeshaji wa mradi wa Panda kwa mwaka 2020. Mradi huu  wa Panda wenye lengo  la kuwawezesha  wasichana  kati ya miaka 18-30 kufikia maendeleo  ya kiuchumi,  kwa kuwapatia mafunzo  ya ujasiriamali  kupitia vipengele vitano  ambavyo ni Kilimo cha mbogamboga, Uokaji wa keki, Upishi,Mapambo na utengenezaji wa kucha ,pamoja na elimu ya kifedha,Utunzaji wa kumbukumbu elimu juu ya ukatili wa kijinsia,na  usimamizi wa biashara. Zaidi ya wasichana 30 wanashiriki katika mradii huu wa Panda kwa kupata mafunzo ya uundaji na utoaji huduma katika jamii zao ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Lengo la mradi wa Panda  ni kuwawezesha na kuwafundisha wasichana  ujuzi mbalimbali na muongozo ili baada ya mafunzo waweze kujiajiri na baadae  kuweza kuwaajiri wengine, lakini pia kupata usimamizi wa kimawazo  katika  biashara kwa walio watangulia kutokana na vipengele  walivyochagua ili kuweza  kuendesha biashara zao vizuri pindi watakapoanza.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni "Wasichana katika biashara kutumia fursa za mafunzo na ushauri ili kujiinua na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi binafsi".

Mradi huu wa panda ni wa miezi 10 na utaambatana na shughuli mbalimbali kama; mafunzo ya vitendo na nadharia, miezi mitatu  ya usimamizi wa kimawazo kwa biashara zao, warsha  itakayolenga kuwakutanisha wasichana wajasiriamali  wachanga  pamoja na sekta binafsi  na za serikali zinazotoa mikopo na mitaji, kampeni ambayo itafanyika kwenye mitandao ya kijamii  kuzungumzia changamoto pamoja na fursa kwa wasichana wajasiriamali.
Her Initiative inashirikiana  na wadau na mashirika mbalimbali katika utoaji wa mafunzo haya wadau hawa ni; Women International First Fund,DOT,Lavy_Product,Mama peridot,Oasis Event, Manka_Cakes,Hedhi Cup,EFM,Reach and Save The Needy,Centum Learning. Tunakaribisha mashirika /Watu binafsi ama taasisi yoyote yenye lengo la kumuinua mtoto wa kike (Msichana) kiuchumi kuungana nasi katika kuendesha na kuendeleza mradii huu.

HER INITIATIVE ni shirika lisilo la kiserikali na si la kibiashara . Shirika  hili limeanzishwa kwa lengo  la kuwaelimisha wasichana katika jamii ili waweze  kujitambua  na kushiriki   katika harakati  zozote za jamii zinazohusu  au kugusa maisha yao. Dhamira kuu ya shirika ikiwa ni kuwaelimisha na kuwapa wasichana  kipaumbele , katika jamii  ili kuchochea  maendeleo ya usawa

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad