HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 16, 2020

BENKI YA CRDB YAZINDUA KAMPENI YA "CHANJA, LIPA, SEPA" NA TEMBOCARDVISA

Mkuu wa Kitengo cha Biashara ya Kadi wa Benki ya CRDB, Farid Seif akifanya malipo kwa kutumia  huduma ya “Chanja, Lipa, Sepa” ya Benki ya CRDB kwa kutumia TemboCardVisa, baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika leo kwenye Duka la Miniso, Mlimani City, jijini Dar es salaam. Benki ya CRDB imezindua rasmi huduma ya “Chanja, Lipa, Sepa” kwa maduka yote yanayokubali malipo ya kadi, ambapo wateja watakao fanya malipo kwa TemboCardVisa na  SimBankingVisa wataweza kufurahia punguzo la bei hadi asilimia 60 kwa manunuzi ya kuanzia shilingi 30,000 katika maduka na migahawa mbalimbali hapa nchini.
Mkuu wa Kitengo cha Biashara na Kadi wa Benki ya CRDB, Farid Seif akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya kufanya malipo kwa kutumia kadi ijulikanayo kama “Chanja, Lipa, Sepa” uliofanyika leo kwenye maduka ya GSM na Miniso, yaliyopo Mlimani City, jijini Dar es salaam.
Meneja wa Mahusiano na Huduma za Uwakala wa Benki ya CRDB, Fadhil Mollel akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya kufanya malipo kwa kutumia kadi ijulikanayo kama “Chanja, Lipa, Sepa” uliofanyika leo kwenye maduka ya GSM na Miniso, yaliyopo Mlimani City, jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad