Mkuu
wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
Mhandisi Lawi Odiero akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Mafia katika
Kampeni ya Mnada kwa Mnada ya kuhamasisha usajili wa Laini za Simu kwa
alama za Vidole katika uwanja wa Kilindoni Wilayani Mafia mkoani Pwani.
Mkuu
wa Kitengo wa Huduma za Bidhaa za Mawasiliano wa TCRA Thadeo Ringo
akizungumza na mwananchi wa Mafia katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada
wilayani Mafia.
Wananchi wakisajili laini za simu kwa alama za vidole.
Mwananchi akisoma kitabu cha muongozo cha TCRA
**********************************
Wakazi
wa wilaya ya Mafia na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi katika
kampeni ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu
Mitandaoni na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Idara ya
Uhamiaji kwa ajili ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa
kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa
kuweka alama za vidole kwa laini za simu.
Kampeni tangu imeanzishwa imekwenda katika Mikoa 17 lengo kuu ni nchi nzima kufikiwa na Kampeni hiyo.
Mkuu
wa Kanda ya Mashariki wa TCRA Mhandisi Lawi Odiero amesema ni fursa kwa
wananchi wa Wilaya ya Mafia kufika katika uwanja wa Kilindoni kwa ajili
ya kusajili kwa alama za vidole pamoja na kujiandikisha kupata usajili
wa vitambulisho vya Taifa kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa
mawasiliano.
Mhandisi
Odiero amesema kuwa Mnada kwa Mnada TCRA ilianzisha ili kutoa fursa ya
Wananchi kuhudumiwa hasa wakati huu usajili wa laini za simu kwa alama
za vidole pamoja Huduma zingine za mawasiliano..
Aidha amesema Kampeni hiyo ni kuimarisha ulinzi katika huduma za simu pamoja kufanya mawasiliano kuwa salama katika nchi.
Amesema
kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya
mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto
wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano nchini.
Mhandisi
Odiero amesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA
wahakikishe wanapata katika usajili wa laini za simu kwa kutumia alama
za vidole na huduma nyinginezo za Mawasiliano hayo.
Hata hivyo amesema kuwakuna
watu wengine wanatumia mawasiliano ya simu bila kujua ambapo Jeshi
Polisi lipo katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada ili kutoa elimu kuhusiana
makosa ya jinai ya matumizi ya simu.
Aidha
amesema Kampeni hiyo ni endelevu katika kuwafikia ikiwa kuhakikisha
kila mwananchi anajisajili laini yake kwa alama za vidole kwa kutumia
kitambulisho cha taifa.Amesema TCRA iko kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi ili mtumie Mawasiliano kwa usalama kutokana na elimu tunayotoa.
Hata hivyo amesema kuwa wananchi wajitokeze katika kujisajili kwa alama za vidole kabla ya Desemba 31.“TCRA
tutahakikisha tunawafikia katika wananchi katika utoaji wa elimu za
utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma
hiyo” amesema.Mhandisi Odiero.
Odiero amesema kuwa Kampeni hiyo imeanza kwa Mkoa wa Pwani hivyo wilaya zote zitakuwa.Nae
Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa TCRA Mabel Masasi amesema kuwa mwitikio
umekuwa mkubwa kwa Wananchi kutaka vitambulisho kwa ajili ya kusajili
laini za simu kwa alama za vidole.
Masasi
amesema kuwa Wananchi wa watumie Kampeni ya Mnada kwa Mnada ya TCRA
kupata elimu na baada ya kuisha Mnada sehemu husika waende katika
mamlaka husika kupata vitambulisho.
No comments:
Post a Comment