HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 4, 2019

DTB BANK YATOA MSAADA WA MAGODORO KWA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA DHI NUREYN, IRINGA

Meneja Masoko wa benki ya DTB-Tanzania,Ndg. Sylvester Bahati (kushoto) akimkabidhi Msimamizi Mkuu wa Kituo cha Watoto Yatima cha Dhi Nureyn, Faidh Said Abri, sehemu ya Msaada wa Magodoro yaliyotolewa na Benki hiyo kwa ajili ya Kituo hicho, kilichopo Mkoani Iringa. Benki ya DTB-Tanzania imetoa Magodoro zaidi ya ishirini, yaliyokuwa yakihitajika sana kituoni hapo, mwishoni mwa wiki.
Meneja Masoko wa benki ya DTB-Tanzania, Sylvester Bahati akiwa ameambatana na baadhi ya Wachezaji wa Timu ya Benki hiyo wanaoshiriki mashindano ya Ligi Daraja la pili, wakati wakizungumza na mmoja wa wasimamizi wa Kituo cha Watoto Yatima cha Dhi Nureyn, kilichopo Mkoani Iringa.
Meneja Masoko wa benki ya DTB-Tanzania, Sylvester Bahati akizungumza kabla ya kukabidhi sehemu ya Msaada wa Magodoro kwa Kituo cha Watoto Yatima cha Dhi Nureyn, kilichopo Mkoani Iringa.
Sehemu ya Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Benki ya DTB wanaoshiriki Ligi Daraja la Pili, wakiwa na baadhi ya Watoto wa Kituo cha Watoto Yatima cha Dhi Nureyn, kilichopo Mkoani Iringa.
Picha ya Pamoja ya Wafanyakazi wa Benki ya DTB pamoja na Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Benki hiyo, nje ya Kituo cha Watoto Yatima cha Dhi Nureyn, kilichopo Mkoani Iringa.
Picha ya Pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad