HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 23, 2019

Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda atembelea Banda la Benki ya Maendeleo TIB wakati wa Maonesho ya Wiki ya Viwanda ya Mkoa wa Pwani

Meneja Mipango na Utafiti wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Samwel Marko (kulia) akitoa maelezo kwa Mgeni Rasmi wa Ufungaji wa Maonesho ya Wiki ya Viwanda ya Mkoa wa Pwani, Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Mizengo Pinda (wapili kulia). Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo.
Mgeni Rasmi wa Ufungaji wa Maonesho ya Wiki ya Viwanda ya Mkoa wa Pwani, Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Mizengo Pinda (wapili kulia) akimsikiliza kwa makini Meneja Mipango na Utafiti wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Samwel Marko (kulia) wakati akitoa maelezo kuhusu uwekezaji uliofanywa na benki hiyo mkoani Pwani. Wengine pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo (katikati), Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani, Bw. Ramadhani Maneno (kushoto) na Meneja Uhusiano na Masoko wa benki hiyo, Bw. Saidi Mkabakuli (wapili kushoto).
Mgeni Rasmi wa Ufungaji wa Maonesho ya Wiki ya Viwanda ya Mkoa wa Pwani, Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Mizengo Pinda (wapili kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Meneja Mipango na Utafiti wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Samwel Marko (kulia) wakati alipotembelea Banda la Benki hiyo. Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo (wapili kushoto) na Meneja Uhusiano na Masoko wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Saidi Mkabakuli (kushoto).
Meneja Mipango na Utafiti wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Samwel Marko (kulia) akipokea Tuzo ya Udhamini wa Maonesho ya Wiki ya Viwanda Mkoa wa Pwani kutoka kwa Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Mizengo Pinda. Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto) na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani, Bw. Ramadhani Maneno (kulia).
Wafanyakazi wa Benki ya Maendeleo TIB walioshiriki ufungaji wa Maonesho ya Wiki ya Viwanda Mkoa wa Pwani wakiwa katika picha ya pamojamara baada ya kukabidhiwa Tuzo ya Udhamini wa Maonesho hayo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad