HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 2, 2019

UBINAFSISHAJI WA KIWANDA CHA NYUZI TABORA BAADA YA KUBAINI HAKIFANYI VIZURI

NA TIGANYA VINCENT
SERIKALI itapitia mkataba wa ubinafsishaji wa Kiwanda cha Nyuzi cha Tabora (New Tabora Textile Tanzania Limited) baada ya kutoridhishwa utendaji wa uzalishaji ili kuchukua hatua mapema ambazo zitasaidia kufanyakazi kwa kiwango chake endapo itabainikiwa wawekwenda kinyume kwa masharti yaliyomo.

Kauli hiyo imetolewa jana na Waziri wa Viwanda na Bisahara Innocent Bashungwa wakati wa ukaguzi wa viwanda mbalimbali mkoani Tabora na kukuta kiwanda cha Nyuzi Tabora kikiwa katika uzalishaji mdogo wakati pamba ya wananchi imejaa mitaani.

Alisema kiwanda hicho kingekuwa kinafanyakazi kulingana na uwezo wake kingesaidia sana kupunguza tatizo la ununuzi wa pamba ya wakulima kususua na kingeongeza uzalishaji wa zao hilo na kukuza uchumi wa Mkoa na Taifa.

Bashungwa alisema kwa kuwa Mmiliki wa Kiwanda hicho ameonekana kuwa na uwezo mdogo na hivyo awe tayari na maamuzi ambayo yatafikiwa baada ya kuangalia mkataba na vigezo alivyopewa wakati ubinafishaji na ikibainika amekiuka Serikali itachukua hatua ili kuongeza tija na utendaji kazi wake.

Alisema wakati wa Mwekezaji huyo na wengine kuendelea kukalia viwanda ambavyo vilitarajiwa kuzalisha kwa ajili ya kukuza uchumi na kutengeza ajira umekwisha na Serikali itachukua hatua.

“Tutangalia Sheria inasemaje na mkataba mlioingia …ili kuangalia njia bora ya kukifanya kiwanda hiki kifanye kazi kwa ajili ya mustakabali mzuri wa wakazi wa Tabora na nchi kwa ujumla” alisema.

Aidha Waziri huyo alivitaja Viwanda vingine ambavyo uzalishaji na utendaji wake sio mzuri ni pamoja na Mwatex na Mutex ambavyo navyo mikataba ya ubinifsishaji wake itachunguzwa kwa ajili ya kuchukua hatua kuvinusuru.

Awali Mbunge wa Tabora Mjini Emmenuel Mwakasaka alisema toka mwaka jana alipotembelea Kiwanda hicho hakuna maendeleo yoyote ambayo yamefanyika na kukifanya kutokuwa na tija kwa vijana na wakazi wa Tabora.

Alisema toka mwaka jana hakuna ajira hata moja iliyoongezeka zaidi ya mfanyakazi mmoja.
 Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa (aliyeshika uzi) akipata maelezo kutoka kwa Katibu wa Kiwanda cha Nyuzi Tabora Pascal Jotham (mwenye shati nyeusi) leo alipokuwa Mkoani Tabora kukagua viwanda mbalimbali. Waziri huyo hauridhishwa na utendaji wa kiwanda hicho na kuahidi kupitia Mkataba wa Ubinafishaji wake.
 Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa (katikati ) akiwa ameshika mmoja ya kitambaa kilichozalishwa na Kiwanda cha Nyuzi Tabora wakati wa ziara yake Mkoani Tabora jana ya kukagua viwanda mbalimbali. Waziri huyo hauridhishwa na utendaji wa kiwanda hicho na kuahidi kupitia Mkataba wa Ubinafishaji wake.

 Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa(kushoto) akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala(kulia) wakati wa ziara yake Mkoani Tabora jana ya kukagua viwanda mbalimbali. Waziri huyo hauridhishwa na utendaji wa kiwanda cha Nyuzi Tabora na kuahidi kupitia Mkataba wa Ubinafishaji wake.
 Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa (mwenye shati nyeupe) akipata maelezo kutoka kwa Katibu wa Kiwanda cha Nyuzi Tabora Pascal Jotham (mwenye shati nyeusi) leo alipokuwa Mkoani Tabora kukagua viwanda mbalimbali. Waziri huyo hauridhishwa na utendaji wa kiwanda hicho na kuahidi kupitia Mkataba wa Ubinafishaji wake. PICHA NA TIGANYA VINCENT

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad