HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 26, 2019

PSPTB yatoa mafunzo kwa Wafanyakazi wa VETA Makao Makuu

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Pancras Bujulu pamoja na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Paul Bilabaye wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa VETA Makao mkuu mara baada ya kumalizika kwa mafunzo yaliyofanyika siku mbili kuanzia Oktoba 25 hadi 26, 2019 katika ukumbi wa ofisi za VETA Makao Makuu, Chang`ombe jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Paul Bilabaye akizungumza jambo wakati wamafunzo kwa Wafanyakazi wa VETA yaliolenga kujenga uelewa wa pamoja kati ya wadau wa ndani ya Mamlaka hiyo (Idara tumizi, kamati za tathmini na Bodi ya Zabuni) juu ya taratibu za kuzingatia katika kutekeleza miradi na shughuli mbalimbali za ununuzi kwa ufanisi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Pancras Bujulu akizungumza wakati wa kufunga mafunzo kwa wafanyakazi wa VETA yaliyoandaliwa na Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) pamoja na VETA Makao Makuu yaliyofanyika katika ukumbi wa VETA Makao Mkuu, Chang`ombe jijini Dar es Salaam leo.

Mshauri wa masuala ya Ununuzi na ugavi, Hamis Mpinda akitoa mafunzo kwa wafanyakazi wa VETA yaliyokuwa yanahusu sheria ya Ununuzi wa Umma pamoja na kanuni zake yaliyofanyika kwa siku mbili kuanzia Oktoba 25 hadi 26, 2019 katika ukumbi wa ofisi za VETA Makao Makuu, Chang`ombe jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Paul Bilabaye akichangia mada wakati wa mafunzo kwa Wafanyakazi wa VETA ambayo pia yalilenga kutatua changamoto katika ununuzi ili kuongeza tija.

Baadhi ya Wafanyakazi wa VETA Makao makuu wakichangia mada wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na PSPTB pamoja na VETA Makao yalikuwa yanahusu sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake yaliyofanyika kwa siku mbili kuanzia Oktoba 25 hadi 26, 2019 katika ukumbi wa ofisi za VETA Makao Makuu, Chang`ombe jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa VETA Makao makuu wakifuatilia mafunzo yaliyoandaliwa na PSPTB pamoja na VETA Makao yalikuwa yanahusu sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake yaliyofanyika kwa siku mbili kuanzia Oktoba 25 hadi 26, 2019 katika ukumbi wa ofisi za VETA Makao Makuu, Chang`ombe jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad