Chama cha Wataalam wa Maendeleo ya jamii nchini CODEPATA kimejidhatiti
katika kuhakikisha wanaifikia jamii na kuwpa elimu ya juu ya
kujitegemea na kutumia fursa na rasirimali walizonazo kujiletea
maendeleo.
Hayo yamesemwa jijini Dodoma na Rais wa Chama cha Maendeleo ya Jamii
CODEPATA Bw. Sunday Wambura katika siku ya tatu ya Kongamano la
Wataalam wa Maendeleo ya Jamii linaloendelea jijini humo.
Bw. Wambura amesema kuwa Chama hicho kimejipanga katika kusimamia pia
maadili ya Kada ya Maendeleo ya Jamii na kuepusha wavamizi wanajiita
Wataalam wa Maendeleo ya Jamii ili kuwa na Kada yenye misingi dhabiti
katika kutekeleza majukuu yake.
“Kuna watu wengi hapa Nchini ambao walikuwa wanajiita wataalamu wa
Sekta hii lakini kwasasa chama kitaweza kuwatambua wataalam sahihi
kutokana na usajili lakini pia wataweka mwongozo utakaotumika katika
utekelezaji wa majukumu ya wataalam wa maendeleo ya jamii.”Aliongeza
Bw. Wambura.
Ameongeza kuwa mwongozo wa Taaluma hiyo uliotolewa na Wizara ya Afya
Idara Kuu Maendeleo ya Jamii kuwa umetolewa kwa wakati kwani utakiwa
nguzo muhimu kwa wataalam hao kuweka vizuri shughuli zao na kutambua
vyema kazi na huduma zinazotolewa na wataalam wa Maendeleo ya Jamii.
Aidha Bw. Wambura amesema awali watu walidhani wataalam hao ni wa
Serikali tu lakini sasa kuna wataalam wa Sekta hiyo wanaopatika na
katika Mashirika Yasiyo Ya Kiserikali na baadhi yao ni wanachama wa
CODEPATA hivyo chama hicho kinafikiria pia kuanzisha mwongozo ambao
utatumika kwa wanachama wote.
“Tutakitumia chama chetu katika kuhakikisha jamii ya kitanzania
inabaili fikra na kujihusisha katika shughuli za maendeleo katika
maeneno yao” alisema Bw. Wambura
Naye Mratibu wa Chama cha Maendeleo ya Jamii Kanda ya Mashariki Bw.
Wanjoke Chinchibera amewataka vijana pamoja na wataalam wa taaluma ya
Maendeleo ya Jamii walio nje ya chama kuendelea kujisajili ili waweze
kufaidika na huduma za chama lakini pia kukipa nguvu chama hicho ili
kiweze kutetea na kulinda maslahi ya taaluma yao.
Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii na Mwanachama wa Chama cha
Wataalam wa Maendeleo ya Jamii CODEPATA Bi. Angela Mvaa amesema kuwa
Chama hicho sio cha Wataalam wa Maendeleo ya Jamii wenye ajira pekee
bali kwa Wataalam wa Maendeleo ya Jamii walio katika ajira rasmi na
walio nje ya ajiri na wale waliomaliza masomo ya Maendeleo ya jamii
nchini.
Wataalam wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii wanakutana Jijini Dodoma
katika Mkutano Mkuu wao wa mwaka kwa lengo la kukumbushana majukumu
yao lakini pia kupata maarifa mapya kutoka mada mbalimbali
zitakazotolewa katika mkutano huo wa siku nne.
No comments:
Post a Comment