HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 22, 2019

BENKI YA CRDB YAKUTANA NA BAADHI YA MAWAKALA WAKE JIJINI DAR LEO

Banki ya CRDB leo imekutana na baadhi ya Watoa huduma ya Uwakala wa Benki hiyo na kufanya  nao kongamano lililoambatana na hafla fupi ikiwa ni muendelezo wa kuadhimisha Mwezi wa Huduma kwa wateja. Pichani ni baadhi wa Mawakala wa Benki hiyo, wakikata keki kama ishara ya kujipongeza kwa huduma bora za kifedha zinazotolewa na mawakala hao, wanaoshuhudia ni Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Cornell Meseyeck (kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Uwanala wa Kibenki wa Benki ya CRDB, Ericky Willy (katikati) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Yolanda Uriyo (kulia).
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Cornell Meseyeck akizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa maalum kwa baadhi ya Mawakala wa Benki ya CRDB, ikiwa ni muendelezo wa kuadhimisha Mwezi wa Huduma kwa wateja, iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Uwakala wa Kibenki wa Benki ya CRDB, Ericky Willyakizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa maalum kwa baadhi ya Mawakala wa Benki ya CRDB, ikiwa ni muendelezo wa kuadhimisha Mwezi wa Huduma kwa wateja, iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Yolanda Uriyo akizungumza katika hafla hiyo.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad