NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA
BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Mwanza limezindua
sherehe na maonyesho ya Maulidi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad S.W.A.
na kuwataka waumini wa dini zote kuhudhuria.
Pia limewataka Watanzania kwa umoja wao kujitokeza kupira kura kwenye
uchaguzi a serikali za mitaa mwaka huu ili kuchagua viongozi waadilifu
weny hofu ya Mungu kwa sababu uimara wa serikali unaanzia chini.
Kaimu Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, Alhaji Sheikhe Hassani Kabeke alisema
jijini humu wakati akizindua sherehe za Maulidi ya kuzaliwa Mtume
Muhammad S.W.A zinazofanyika kitaifa mkoani humu.
Alisema wananchi na wakazi wa Jiji la Mwanza waislamu na wasio
waislamu wajitokeze kwenye maulidi hayo ya kuzaliwa kwa Mtume na
waonyeshe ukarimu wao kwa wageni wa ndani na nje ya nchi
watakaohudhuria sherehe hizo ambazo mgeni rasmi atakuwa Mufti Abubakar
Zuberi.
Sheikhe Kabeke alieleza kuwa Novemba 9, kabla kutafanyika matembezi ya
amani (Zafa) yatakayoongozwa na Ngamia wawili na kupokewa na Mutfi,
yakianzia BAKWATA mkoa kupitia barabara ya Nyerere hadi Viwanja vya
Furahisha, Manispaa ya Ilemela ambapo kabla maandamano hayo kutakuwa
na siku maalumu ya kuombea nchi idumu katika amani na utulivu.
“Tumezindua rasmi leo maonyesho na sherehe za maulidi ya Mtume
Muhammad S.A.W ambayo ni siku yake ya kuzaliwa na kilele chake
kitakuwa Novemba 9, mwaka huu, kutakuwa na maonyesho ya shughuli za
kijamii,upimaji wa kisukari,macho, shinikizo la damu na uchangiaji wa
damu wa hiari unaolenga kukusanya chupa 8,000 ili kuokoa maisha ya
watu kama alivyofanya Mtume,”alisema Sheikhe Kabeke.
Sheikhe huyo wa mkoa aliwahamasisha wananchi wa jiji hili kufanya
usafi kwenye mitaa yao, makazi, barabara na kupaka rangi nyumba huku
akiwashauri waumini wa dini ya Kiislamu kuunda vikundi vya kupita
nyumba kwa nyumba ili kuwaalika waumini wa dini zingine washiriki
maulidi.
Aidha, kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba
24, aliwataka wanasiasa wasiharibu nchi kwa uchu wa madaraka, bali
wafahamu kuna watanzania zaidi ya watu milioni 55 ilhali vyama vyao
vikiwa na wananchama wasiozi milioni 30.
Pia aliwahamiza watanzania hasa wa Mwanza kujitokeza kwa wingi
kuchagua viongozi waadilifu na wenye hofu ya Mungu kwani uimara wa
serikali unaanzia chini na itakuwa busara wanasiasa wakaongeza juhudi
ili uchaguzi ufanyike kwa amani,usalama na utulivu badala ya
kusababisha migogoro inayoweza kuharibu nchi.
Sheikhe Kabeke alionya wananchi kuwa, kuwachagua watu wasio na
uadilifu ni kukaribisha matatizo kwenye jamii na hivyo siku ikifika
wachague viongozi wenye mshikamano na uadilifu watakaoimarisha
maendeleo yaliyopatikana chini ya serikali ya awamu ya tano.sssss
Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Alhaji Sheikhe Hassani Kabeke akizungumza na Waislamu kwenye Ukumbi wa Sheikh Salum Ferej kabla ya kuzindua maulidi ya kitaifa ya kuzaliwa Mtume Muhammad S.A.W.
Kaimu Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza Alhaji sheikhe Hassani Kabeke akipandisha bendera ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) ikiwa ni ishara ya kuzindua maonyesho na sherehe za Maulidi ya Mtume Muhammad S.A.W yanayofanyika kitaifa jijini humu.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakishiriki pamoja na kaimu sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, alhaji Hassani Kabeke kuimba qaswida wakati wa uzinduzi wa sherehe nza maulidi zilifanyika kwenye ukumbu wa Sheihe Salum Ferej jana .
No comments:
Post a Comment