HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 30, 2019

WAZEE WAIOMBA SERIKALI KUWAPATIA PENSHENI JAMII

 Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii  Dkt. John Jingu akifungua kongamano la wazee lililofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu Mkoani Mtwara katika mfulululizo wa maadhimisho ya Kimataifa ya Wazee.
 Kamishna wa Ustawi wa Jamii Nchini kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii  Dkt. naftari Ngondi   akifafanua jambo wakati wa  kongamano la wazee lililofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu Mkoani Mtwara.
 Baadhi ya washiriki kongamano la wazee linaloendelea katika ukumbi wa Benki Kuu Mkoani Mtwara.
Mzee Seifu Nantapika Katibu Mtandao wa Wazee Mkoa wa Mtwara akitoa salamu kwa wazee washiriki kongamano la wazee lililofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu Mkoani Mtwara

Baraza la Wazee limeiomba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwasaidia wazee kwa kuwapatia pensheni jamii itakayowasaidia katika mahitaji yao ya kila siku kwa wazee ambao hawakuwa katika ajira rasmi.

Hayo yamebainika leo mkoani Mtwara wakati wa uzinduzi wa Kongamano la Wazee kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani lililofanyika katika ukumbi wa Benki ya Tanzania.

Akizungumza mara baada ya Kongamano hilo Katibu wa Baraza la Wazee la Halmashauri ya Mji wa Kahama Mzee Anderson Lyimo amesema kuwa wazee wamelitumikia taifa katika Nyanja mbalimbali hivyo ni suala la muhimu kwa Serikali kutafakari na kuwapatia wazee pensheni jamii itakayowasaidia kutatua changamoto ndogondogo za kimaisha.

Mzee Lyimo ameongeza kuwa pensheni ya jamii kwa wazee itawasaidia wazee kuondokana na utegemezi kwa jamii hasa kuondokana na wimbi la wazee ombaomba ambalo kwa kiasi kikubwa hutokana na wazee kukosa fedha za kujikimu kwa mahitaji yao madogo madogo.

“Tunakuomba Mhe. Rais Magufuli tukumbuke katika suala la pensheni jamii kwetu sisi wazee itatusaidia sana kwa mfano wenzetu wa Zanzibar wanapata elfu 20 angalau kupata kuliko kukosa kabisa” alisisitiza Mzee Lyimo.

Mzee Lyimo amesisitiza kuwa jamii inawajibu wa kuwalea na kuwatunza wazee kwa asilimia kubwa na kuwaasa vijana kutowatelekeza wazazi wao wakati wanapozeeka na wajue kuwa ni wajibu wao kuwalea na kuwatunza wazee kama wao walivyotunzwa wakiwa watoto.  

Akifungua Kongamano hilo Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu amesema kuwa Kongamano hilo litumike kutafakari kwa jinsi gani taifa litafanya kuwalea na kuwatunza wazee na kupata njia sahihi za kupambana na changamoto zinazowakabili.

Dkt. Jingu ameongeza kuwa ni muhimu sana kwa taifa kujadili suala la kuwaenzi na kuwatunza wazee pamoja na kuhakikisha wanakuwa na ustawi mzuri katika maisha yao ili waendelea kutoa mchango wao katika ujenzi wa taifa.

“Naomba tujadilia pia wajibu wa jamii katika kuwatunza na kuwaenzi wazee kama wazazi wao ndugu na jamaa waliochangia nguvu zao katika ujenzi wa taifa letu” alisema Dkt. Jingu

Dkt. Jingu ametaja jitihada hizo kuwa ni pamoja na Sera ya matibabu bure kwa wazee, uwepo wa mabaraza ya wazee na mapitio ya Sera ya wazee ili kuhakikisha kuwa inajitosheleza lakini pia Serikali ina makao 17 ya wazee ambayo yanapokea wazee wasiokuwa na ndugu wala jamii ya kuwahudumia.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Chama cha Wazee na Wastaafu mkoa wa Arusha Bi. Miriam Urio amewataka vijana nchini kuachana na vitendo vya imani za kishirikiana kusababisha vifo kwa wazazi wao kwasababu ya uzee bali wawatunze na kuwalea wazee wao kama wao walivyowatunza wakiwa watoto. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad