WATAFITI wa dawa za binadamu wamehimizwa kufanya tafiti ambazo zitasaidia
uzalishaji wa dawa ambazo zitamlinda mtumiaji na kuepusha athari zinazoweza
kujitokeza baada ya matumizi.
Ameyasema hayo leo Mkurugenzi wa
Kuratibu na kukuza utafiti wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya
Binadamu (NIMR) Dkt.Paul Kazyoba katika mkutano wa mwaka wa pili wa Smert
project uliofanyika katika ofisi za TMDA jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Dkt.Kazyoba amewataka Wananchi
kujijengea utaratibu wa kuuliza kama tafiti za afya zimepitia utaratibu hivyo
taasisi ndogondogo zinazofanya utafiti wa afya zijijengee uwezo wa kuweza
kutathimini maadili ya tafiti zenyewe.
Lengo kubwa la kuwa na Smert project ni kuhakikisha Mwananchi analindwa
katika usalama wake kwenye matumizi ya dawa.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha NIMR_Mbeya, Mtafiti Mkuu wa Mradi
wa Smert (Tanzania_Uk) Dkt.Nyanda Ntinginya amesema kuwa mradi huo ulianzishwa
kwa malengo ya kuimarisha utendaji kazi wa kamati za naadili za taasisi pamoja
na utendaji kasi wa kamati za kikanda za utafiti.
“Kabla ya mradi huu hatujafanya kulikuwa na changamoto ya muda mrefu
kutumiwa kabla ya mradi kuruhusiwa kwenda kufanyiwa utafiti”.Amesema Dkt.Ntinginya,
Mkurugenzi wa Kuratibu na kukuza utafiti wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Dkt.Paul Kazyoba (kulia) akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano wa Mwaka wa pili wa Smert project uliofanyika katika ofisi za (TMDA) leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurungenzi wa Dawa na vifaa tiba wa Mamlaka wa Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Akida Khea (kulia) akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa pili wa Smert project uliofanyika katika ofisi za (TMDA) leo jijini Dar es Salaam.
Meneja Mawasiliano na Elimu kwa Umma,wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA),Gaudensia Simwanza akizungumza wakati alipokuwa akitambulisha sehemu ya viongozi wa ngazi mbalimbali katika ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa pili wa Smert project uliofanyika katika ofisi za TMDA leo jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa habari wakimsikiliza Kaimu Mkurungenzi wa Dawa na Wifaa tiba wa Mamlaka wa Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Akida Khea (kulia).
(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)
(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)
No comments:
Post a Comment