HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 2, 2019

PROGRAMU YA MAFUNZO WA KWANAWAKE KUFANYIKA NCHINI KOTE

Mkufunzi Taasisi ya Purple Planet,Violet Konyani akizungumza na waandishi wa habari jijni Dar es Salaam leo wakati wa kutamulisha programu ya mafunzo kwa wanawake yatakayo fanyika katika mikoa kikanda nchini kote.SHIRIKA lisilo la kiserikali linalojihusiasha na maendeleo ya wanawake kijamii na kiuchumi nchini Purple Planet imetambulisha programu ya mafunzo kwa mwanamke sahihi kwa mwaka 2019 ambayo itahamasisha wanawake kwa nadharia na vitendo kuelekea uchumi wa Viwanda.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa kampuni ya Purple Planet, Hilda Kisoka amesema kuwa Programu hii itawakusanya wanawake pamoja kwaajili ya kuwainua kiuchumi.

"Programu hii kwaajili ya mwanamke sahihi kwa 2019 italenga kuhamasisha wanawake na inalengo la kugusa makundi zaidi ya wanawake 2000 katika sekta binafsi kwa awamu ya kwanza katika mikoa mbalimbali hapa nchini".

Hilda amesema kuwa wanawake wa kanda mbalimbali hapa nchini wajiandae kwaajili ya Program hiyo ambayo itakuwa katika mikoa mbalimali kulingana na kanda zao. 

Kanda ya Pwani ambayo inajumuisha mikoa ya Pwani na Morogoro itafanyika jijini Dar es Salaam, Kanda ya kati inayojumuisha mikoa ya Dodoma na Singida programu hiyo itafanyika jijini Dodoma, kanda ya kati kasikazini inayojumisha mikoa ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha itafanyika Arusha, Kanda ya ziwa itafanyika jijini Mwanza.

Hilda amesema kuwa kampuni ya purple planet kwa awamu ya kwanza itaanza kutoa mafunzo kwa miezi mitatu kisha itaendelea tena kwa awamu nyingine.

Program ambazo watakazotoa mafunzo ni fasheni na kubuni ambayo itatolewa na speshoz, Mapishi ambayo yatafanyika kwa Maanjumati na BRAGEN CATERING, Mambo ya Saloon na urembo, itafanyika Dage na Lavy, Uokaji wa Keki itafanyika Melisa School of Bake, Upangaji wa Matukio na urembo yatafanyika Sabrionce event na Bragen, na The Event Crop COMESAVE Dodoma.

Pia usindikaji wa vyakula na bidhaa za majumbani itafanyika kusiga Product, First R&R Supermarkets kwaajili ya masoko, ufugaji na kilimo itafanyika Malemo Farm, Ufugaji wa kuku nutafanyika kuku Project pamoja na kuandda Rasilimali watu itafanyika Top Taget na kazi point.

Hilda amesema katika kufanikisha hiyo Purple Plane wanashirikia na mamlaka za serikali ili kuleta ufanisi katika mafunzo mbalimbali yatakayotolewa ikiwemo, NEEC, JUWADA, SIDO, GS1,TBS, na UTT. 
Hata hiyo Hila amesema kuwa changamoto kubwa wanayokumana nayo ni kuwa na wanawake wachache ambao wanahitaji kujikwamua kiuchumi.

Pia amewaalika wanawake kuhudhulia programu ya mafunzo hayo ili waweze kutatua changamoto zao za masoko, ujuzi na mitaji hata changamoto za kijamii kwa kutumia rasilimali walizonazo bila kusubiri serikali kuelekea uchumi wa viwanda.
,Mkurugenzi wa kampuni ya Purple Planet, Hilda Kisoka akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kutamulisha uprogramu ya m,afunzi wa wanawake ili kujikwamua kiuchumi na changamoto za kijamii. kulia ni  Mkufunzi Taasisi ya Purple Planet,Violet Konyani.

Mkufunzi wa mafunzo yanayotolewa na Purple Planet, Breatice Nyalandu  akizungumza na waandishi wa badari wakati wa kutambulisha programu ya mafunzo kwa wanawake yatakayofanyika nchini kote. Amesema mafunzo hayo hayatabagua dini yatakuwa kwa watu wote. 
Mkufunzi wa Shirika la Purple Planet, Sara Pima akifafanua jamo wakati wa kutambulisha wa programu ya mafuzo kwa wanawake wote hapa nchini yatakayomwenzesha mwanamke kujikwamu kiuchumi na changamoto ja kijamii. amafunzo yatakayotolewa kwenye kanda za mikoa yote ya hapa nchini.

Baadhi ya wajumbe na viongozi wa Purple Planet

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad