Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Katika kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa soko la pamba mkoa wa
Simiyu umeandaa mkakati maalum wa miaka mitano (2019-2024) wa
mapinduzi ya kilimo cha zao hilo ili kujibu changamoto zinazowakabili
wakulima wa pamba.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka
katika Mkutano wa Wadau wa Pamba uliofanyika uliofanyika Agosti 28,
2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi
ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka
mitano 2019-2014,
Akifungua Mkutano huo Mtaka amesema upo umuhimu mkubwa kwa Mkoa wa
Simiyu kuwa na kiwanda/viwanda vya kuongeza thamani ya zao la pamba
ikiwemo viwanda vya nguo kama suluhisho la soko la pamba kwa wakulima.
“Kama hatutakuwa na viwanda vinavyoongeza thamani kwenye pamba,hata
kama tukiongeza uzalishaji, itafika mahali tutatukanana tu, maana
pamba itakuwa nyingi na hakuna mtu wa kukununua na wanaonunua wanajua
hatuna kwa kuipeleka, kwa hiyo ni lazima tukubaliane na ndiyo maana
tukasema tuje na mkakati huu unaoanza na mkulima kuanzia kwenye
kulima” alisema Mtaka.
Aidha, Mtaka amesema ili kuwasaidia wakulima katika upatikanaji wa
mikopo ni vema benki zikaweka utaratibu rafiki wa kutoa mikopo kwa
wakulima huku akitoa wito kwa Benki Kuu kupitia Kurugenzi ya Sera
kuandika maandiko ya miradi ya mazao ya mikakati likiwemo pamba ambayo
yatasaidia katika kuyaongezea thamani mazao hayo.
Akiwasilisha mkakati huo kwa wadau wa pamba mkoani Simiyu, Katibu
Tawala Msaidizi wa Mipango na Uratibu Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus
Weginah amesema uongezaji thamani kwenye pamba mkoani Simiyu bado liko
chini; ambapo kwa sasa kinachofanyika ni kutengenisha pamba nyuzi,
mbegu na kuchuja mafuta, huku akibainisha kuwa matarajio ya mkoa ni
kwenda kwenye hatua nyingine zaidi ya kuchambua pamba.
Pamoja na kuongeza thamani ya zao la pamba wadau wa pamba wametoa
maoni mbalimbali katika kuboresha kilimo cha Pamba ili kiwe chenye
tija na kubainisha kuwa “Ili tuweze kuboresha kilimo cha pamba ni
lazima teknolojia zitakazokabiliana na changamoto za mabadiliko ya
tabianchi, wadudu na magonjwa” alisema Epifania Temu kutoka Taasisi ya
Utafiti wa Kilimo(TARI) Ukiriguru
“Mbegu ndiyo msingi wa tija ya pamba inayopaswa kuzalishwa kwenye
soko, hivyo kwenye eneo lililokubaliwa kuzalisha mbegu kama Meatu na
Igunga ginners (wenye viwanda vya kuchambua pamba) watakaokununua
pamba ya eneo wapewe jukumu la kuzalisha mbegu ili kuwa na mwendelezo
wa mbegu bora” alisema Mkondo Cornelius Afisa Kilimo Mkuu, Wizara ya
Kilimo.
Mkurugenzi wa Miradi kutoka Gatsby Africa, Samweli Kilua ametoa wito
kwa wadau wote kuhakikisha kila mdau anatimiza wajibu wake katika
kuhakikisha mkakati huo unatekelezwa kwa ufanisi katika kuboresha
kilimo cha pamba.
Akifunga kikao Katibu Tawalawa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini
amesema mkakati wa mapinduzi ya kilimo cha pamba Mkoani Simiyu
utatekelezwa kwa vitendo na akazitaka Taasisi za fedha, viongozi na
wataalam wanaosimamia wakulima, vyama vya ushirika na wadau wengine
waanze mazungumzo ili mkakati huo utakapoanza kutekelezwa kuwe na
uelewa wa pamoja kwa wadau wote.
Mkutano wa kuboresha mkakati maalum wa miaka mitano (2019-2024) wa
mapinduzi ya kilimo cha pamba ulijumuisha wadau mbalimbali wa kilimo
cha pamba ambao ni pamoja na viongozi wa Chama na Serikali Mkoa wa
Simiyu, Watalaam wa kilimo kutoka Taasisi za Utafiti wa Kilimo, Wizara
ya Kilimo, Halmashauri na Mkoa, Watendaji wa Taasisi za Fedha,
viongozi wa vyama vya msingi vya ushirika.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Wadau mbalimbali wa kilimo cha pamba katika ufunguzi wa Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na Wadau mbalimbali wa kilimo cha pamba katika Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Komredi Kheri James akitoa salamu zake kwa Wadau mbalimbali wa kilimo cha pamba katika Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Komredi Enock Yakobo akizungumza na Wadau mbalimbali wa kilimo cha pamba katika Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wadau wa kilimo cha pamba wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mkurugenzi wa Miradi wa Gatsby Africa, Samweli Kilua akitoa taarifa ya namna shirika hilo lilivyoshiriki katika uaandaaji wa Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, kwenye mkutano wa kuboresha mkakati huo uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mkurugenzi wa Miradi kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wwa Mataifa(UNDP), Amon Manyama akichangia hoja Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Mipango na Uratibu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah akiwasilisha mkakati wa maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, katika Mkutano wa kuboresha Mkakati huo uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mmoja wa Wawakilishi wa Wakurugenzi na wamiliki wa Viwanda
vya Kuchambua pamba kutoka kiwanda cha Alliance Ginneries Ltd,
akichangia hoja katika Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa
Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi
cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Katika kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa soko la pamba mkoa wa
Simiyu umeandaa mkakati maalum wa miaka mitano (2019-2024) wa
mapinduzi ya kilimo cha zao hilo ili kujibu changamoto zinazowakabili
wakulima wa pamba.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka
katika Mkutano wa Wadau wa Pamba uliofanyika uliofanyika Agosti 28,
2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi
ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka
mitano 2019-2014,
Akifungua Mkutano huo Mtaka amesema upo umuhimu mkubwa kwa Mkoa wa
Simiyu kuwa na kiwanda/viwanda vya kuongeza thamani ya zao la pamba
ikiwemo viwanda vya nguo kama suluhisho la soko la pamba kwa wakulima.
“Kama hatutakuwa na viwanda vinavyoongeza thamani kwenye pamba,hata
kama tukiongeza uzalishaji, itafika mahali tutatukanana tu, maana
pamba itakuwa nyingi na hakuna mtu wa kukununua na wanaonunua wanajua
hatuna kwa kuipeleka, kwa hiyo ni lazima tukubaliane na ndiyo maana
tukasema tuje na mkakati huu unaoanza na mkulima kuanzia kwenye
kulima” alisema Mtaka.
Aidha, Mtaka amesema ili kuwasaidia wakulima katika upatikanaji wa
mikopo ni vema benki zikaweka utaratibu rafiki wa kutoa mikopo kwa
wakulima huku akitoa wito kwa Benki Kuu kupitia Kurugenzi ya Sera
kuandika maandiko ya miradi ya mazao ya mikakati likiwemo pamba ambayo
yatasaidia katika kuyaongezea thamani mazao hayo.
Akiwasilisha mkakati huo kwa wadau wa pamba mkoani Simiyu, Katibu
Tawala Msaidizi wa Mipango na Uratibu Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus
Weginah amesema uongezaji thamani kwenye pamba mkoani Simiyu bado liko
chini; ambapo kwa sasa kinachofanyika ni kutengenisha pamba nyuzi,
mbegu na kuchuja mafuta, huku akibainisha kuwa matarajio ya mkoa ni
kwenda kwenye hatua nyingine zaidi ya kuchambua pamba.
Pamoja na kuongeza thamani ya zao la pamba wadau wa pamba wametoa
maoni mbalimbali katika kuboresha kilimo cha Pamba ili kiwe chenye
tija na kubainisha kuwa “Ili tuweze kuboresha kilimo cha pamba ni
lazima teknolojia zitakazokabiliana na changamoto za mabadiliko ya
tabianchi, wadudu na magonjwa” alisema Epifania Temu kutoka Taasisi ya
Utafiti wa Kilimo(TARI) Ukiriguru
“Mbegu ndiyo msingi wa tija ya pamba inayopaswa kuzalishwa kwenye
soko, hivyo kwenye eneo lililokubaliwa kuzalisha mbegu kama Meatu na
Igunga ginners (wenye viwanda vya kuchambua pamba) watakaokununua
pamba ya eneo wapewe jukumu la kuzalisha mbegu ili kuwa na mwendelezo
wa mbegu bora” alisema Mkondo Cornelius Afisa Kilimo Mkuu, Wizara ya
Kilimo.
Mkurugenzi wa Miradi kutoka Gatsby Africa, Samweli Kilua ametoa wito
kwa wadau wote kuhakikisha kila mdau anatimiza wajibu wake katika
kuhakikisha mkakati huo unatekelezwa kwa ufanisi katika kuboresha
kilimo cha pamba.
Akifunga kikao Katibu Tawalawa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini
amesema mkakati wa mapinduzi ya kilimo cha pamba Mkoani Simiyu
utatekelezwa kwa vitendo na akazitaka Taasisi za fedha, viongozi na
wataalam wanaosimamia wakulima, vyama vya ushirika na wadau wengine
waanze mazungumzo ili mkakati huo utakapoanza kutekelezwa kuwe na
uelewa wa pamoja kwa wadau wote.
Mkutano wa kuboresha mkakati maalum wa miaka mitano (2019-2024) wa
mapinduzi ya kilimo cha pamba ulijumuisha wadau mbalimbali wa kilimo
cha pamba ambao ni pamoja na viongozi wa Chama na Serikali Mkoa wa
Simiyu, Watalaam wa kilimo kutoka Taasisi za Utafiti wa Kilimo, Wizara
ya Kilimo, Halmashauri na Mkoa, Watendaji wa Taasisi za Fedha,
viongozi wa vyama vya msingi vya ushirika.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Wadau mbalimbali wa kilimo cha pamba katika ufunguzi wa Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na Wadau mbalimbali wa kilimo cha pamba katika Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Komredi Kheri James akitoa salamu zake kwa Wadau mbalimbali wa kilimo cha pamba katika Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Komredi Enock Yakobo akizungumza na Wadau mbalimbali wa kilimo cha pamba katika Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wadau wa kilimo cha pamba wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mkurugenzi wa Miradi wa Gatsby Africa, Samweli Kilua akitoa taarifa ya namna shirika hilo lilivyoshiriki katika uaandaaji wa Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, kwenye mkutano wa kuboresha mkakati huo uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mkurugenzi wa Miradi kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wwa Mataifa(UNDP), Amon Manyama akichangia hoja Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Mipango na Uratibu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah akiwasilisha mkakati wa maalum wa Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu katika kipindi cha miaka mitano 2019-2014, katika Mkutano wa kuboresha Mkakati huo uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
Mmoja wa Wawakilishi wa Wakurugenzi na wamiliki wa Viwanda
vya Kuchambua pamba kutoka kiwanda cha Alliance Ginneries Ltd,
akichangia hoja katika Mkutano wa kuboresha Mkakati maalum wa
Mapinduzi ya Kilimo cha Zao la Pamba Mkoa wa Simiyu, katika kipindi
cha miaka mitano 2019-2014, uliofanyika Agosti 28, 2019 Mjini Bariadi.
No comments:
Post a Comment