HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 26, 2019

RAIS DKT. SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI WA WIZARA YA NCHI OFISI YA RAIS UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA ZANZIBAR



RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Zanzibar, wakatiu wa mkutano wa Utekelezaji wa Bajeti kwa mwezi Julai 20 hadi Juni 2019 na Mpango Kazi Mpya kwa mwaka 2019 -2020, uliofanyika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.(Picha na Ikulu)
KAIMU Waziri wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora Zanzibar Mhe. Khamis Juma Mwalim akiwasilisha ripoti ya Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi wa Wizara hiyo kwa mwezi Julai 2018 hadi Juni 2019 na mpango kazi kwa mwaka 2019 -2020, wa Wizara hiyo, wakati wa mkutano huo ukiongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kushoto Mshauri wa Rais Pemba Mhe.Dk. Maua Abeid Daftari na na kulia Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee.
KATIBU Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ndg. Yakout Hassan Yakout, akisoma Utekelezaji wa Bajeti  na Mpango Kazi kwa mwezi Julai 2018 hadi 2019, na kuwasilisha mpango kazi wa mwaka 2019-2020, kushoto Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi.

WATENDAJI wa Idara za Wizara ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Zanzibar, wakifuatilia Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi kwa mwezi wa Julai 2018 hadi Juni 2019 na Mpango kazi kwa mwaka 2019 hadi 2020, mkutano huo umefanyika ukumbi Ikulu Zanzibar.(Picha na Ikulu)   

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad