HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, July 13, 2019

Sagini aitaka VETA kupeka mashine Simiyu

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Jumanne Sagini amesema bidhaa zinazozalishwa na VETA wapeleke kwa wakulima ili kuweza kutatua changamoto zao ikiwa pamoja na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo.

Sagini aliyasema hayo wakati alipotembelea Banda la VETA katika Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.amesema wakulima wanahitaji mashine mbalimbali ambazo VETA mnazalisha hivyo zisiishie katika Maonesho.

Amewataka VETA kwenda na mashine hizo na kuziuza kwa wakulima wa Simiyu katika Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika mkoani humo.
Sagini amesema kuwa VETA wanafanya ugunduzi katika nyanja mbalimbali ambazo zikitumiwa vizuri kutarahisha wakulima kukua kiuchumi kutokana na vitendea kazi kutoka VETA.
Aidha amesema kuwa mashine za VETA zisimbazwe kwani gharama itakuwa rahisi kwa wakulima kumudu kuliko mashine za nje.
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Jumanne Sagini akipata maelezo kutoka VETA kwa mwanafunzi wenye mahitaji Maalum vitu wanavyotengeneza wakati alipotembelea Banda la VETA katika Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Jumanne Sagini akipata maelezo kuhusiana na mashine ya kuchakata majani kwa ajili ya Mifugo wakati alipotembelea Banda la VETA katika Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Jumanne Sagini akizungumza na waandishi habari kuhusiana vitu alivyoona katika banda la VETA katika Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mashine iliyundwa na Watu Wenye mahitaji Maalum kwa kushirikiana na Mwalimu wao wa VETA Chang'ombe.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad