Naibu Waziri Mhe.Juliana Shonza (kushoto) akimkabidhi zawadi ya mchezaji
bora mchezaji
kutoka Timu ya Yanga Mrisho Ngassa (kulia) mara baada kumalizika kwa mechi ya
Tamasha la Michezo lililoandaliwa na Kanisa la Baptism la mkoa huo nakufanyika
leo katika uwanja wa Jamhuri.
Naibu Waziri Mhe.Juliana Shonza akimkabidhi kocha wa timu ya Mawenzi
Market (ambaye jina lake halikufamika) zawadi ya mchezaji bora wa timu hiyo kwa
niaba ya mchezaji huyo mara baada ya kumalizika kwa mechi yao iliyofanyika
katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro,katikaTamasha la Michezo lililokuwa
limendaliwa na kanisa la Baptist la Mkoani huo.
Naibu Waziri Mhe.Juliana Shonza (kushoto) akiteta jambo na Mchungaji Jerry
Watt wa Kanisa la Baptist la Mkoani Morogoro aliyeandaa Tamasha la Michezo
wakati wa mechi kati ya Timu ya Yanga na Timu ya Mawenzi Market ya Mkoani hapo
walipokuwa wakicheza leo katika Uwanja wa Jamhuri.
Mchungaji wa Kanisa la Baptist la Mkoani Jerry Watt akihubiri neno la mungu
katika Tamasha la Michezo lililofanyika leo katika uwanja wa Jamhuri Mkoani
Morogoro,Tamasha hilo liliandaliwa na kanisa hilo na lilikuwa na mechi kati ya
timu ya Yanga na timu ya Mawenzi Market ya mkoa huo.
Naibu Waziri Mhe.Juliana Shonza akitizama kombe la ushindi kabla ya
kulikabidhi kwa timu ya Yanga baada ya kuibuka washindi katika Tamasha la
Michezo lililoandaliwa na kanisa la Baptist Michezo la Mkoa wa Morogoro na
kufanyika leo katika Uwanja wa Jamhuri.
Kwaya ya Kanisa la Baptist kutoka Marekani ikiimba wimbo wakumsifu mungu
katika Tamasha la Michezo lililoandaliwa na Kanisa hilo leo katika Uwanja wa
Jamhuri Mkoani Morogoro
No comments:
Post a Comment