Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Mzee Mkongea Ali ameweka jiwe la Msingi mradi wa ujenzi wa tanki na mfumo wa usambazaji maji katika maeneo ya Pugu, Gongo la Mboto, Pugu Station, Air Wing, Ukonga na Majohe.
Kiongozi huyo pia amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mgema kuhakikisha malighafi zote zinazotumika katika mradi wa maji Pugu yanafanyiwa vipimo kubaini ubora wake ili kuhakikisha mradi huo unakuwa imara na kudumu kwa muda mrefu.
Kauli hiyo ameitoa leo wakati akiweka jiwe la msingi katika mradi huo ambao unatekelezwa kwa kutumia fedha za ndani za Mamlaka ya Majisafi na majitaka Dar es Salaam DAWASA.
Mmradi huo umegharimu Sh. Bilioni 7.3 ambapo Mzee Mkongea amemshukuru Rais Magufuli kwa kuhakikisha watu wanapata MajiSafi na salama.
Akizungumza baada ya kuzinduliwa kwa mradi huo, Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema mradi huo unatekelezwa na mamlaka hiyo ikiwa ni katika jitihada za kuboresha huduma za maji kwenye maeneo yaliyokuwa hayana mtandao wa maji safi lengo ni kufikia asilimia 95 ya wakazi mnamo 2020.
"Mradi huu unatarajiwa kusambaza maji katika maeneo ya Pugu, Majohe, Gongo la mboto, Bangulo, Ukonga-Airwing, Kigogo na Buyuni/Chanika na maeneo jirani pia mradi utaendelea kupanuliwa kulingana na upatikanaji wa fedha", amesema
Ameongeza kuwa bomba Kuu litakuwa na uwezo wa kusafirisha kiwango cha maji kipatacho lita 2,880,000 kwa siku ambapo wakazi wapatao 450,000 wanatarajiwa kunufaika na mradi huo pamoja na maunganisho mapya ya wateja zaidi ya 50,000 yatafanyika mara baada ya kukamilika kwa mradi.
Kiongozi huyo pia amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mgema kuhakikisha malighafi zote zinazotumika katika mradi wa maji Pugu yanafanyiwa vipimo kubaini ubora wake ili kuhakikisha mradi huo unakuwa imara na kudumu kwa muda mrefu.
Kauli hiyo ameitoa leo wakati akiweka jiwe la msingi katika mradi huo ambao unatekelezwa kwa kutumia fedha za ndani za Mamlaka ya Majisafi na majitaka Dar es Salaam DAWASA.
Mmradi huo umegharimu Sh. Bilioni 7.3 ambapo Mzee Mkongea amemshukuru Rais Magufuli kwa kuhakikisha watu wanapata MajiSafi na salama.
Akizungumza baada ya kuzinduliwa kwa mradi huo, Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema mradi huo unatekelezwa na mamlaka hiyo ikiwa ni katika jitihada za kuboresha huduma za maji kwenye maeneo yaliyokuwa hayana mtandao wa maji safi lengo ni kufikia asilimia 95 ya wakazi mnamo 2020.
"Mradi huu unatarajiwa kusambaza maji katika maeneo ya Pugu, Majohe, Gongo la mboto, Bangulo, Ukonga-Airwing, Kigogo na Buyuni/Chanika na maeneo jirani pia mradi utaendelea kupanuliwa kulingana na upatikanaji wa fedha", amesema
Ameongeza kuwa bomba Kuu litakuwa na uwezo wa kusafirisha kiwango cha maji kipatacho lita 2,880,000 kwa siku ambapo wakazi wapatao 450,000 wanatarajiwa kunufaika na mradi huo pamoja na maunganisho mapya ya wateja zaidi ya 50,000 yatafanyika mara baada ya kukamilika kwa mradi.
Kiongozi
wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2019 Mzee Mkongea Ali akiweka jiwe
la msingi la mradi wa ujenzi wa Tenki na Mfumo wa Usambazaji wa Maji
Pugu-Gongolamboto uliofanyika leo katika eneo la Pugu jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja akisoma risala wakati
wa kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa Tenki na Mfumo wa
Usambazaji wa Maji Pugu-Gongolamboto uliofanyika leo katika eneo la Pugu
jijini Dar es Salaam.
Kiongozi
wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2019 Mzee Mkongea Ali akizungumza na
wananchi waliohudhuria kwenye uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa
ujenzi wa Tenki na Mfumo wa Usambazaji wa Maji Pugu-Gongolamboto
uliofanyika leo katika eneo la Pugu jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja akionesha
namna mradi wa ujenzi wa Tenki na Mfumo wa Usambazaji wa Maji
Pugu-Gongolamboto utakavyofanya kwa Viongozi wa Mbio za mwenge mwaka
2019.
No comments:
Post a Comment