HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 20, 2019

TPDC YAMPA TUZO PROF. MARK MWANDOSYA

HIVI Karibuni Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), lilifanya Maadhimisho ya Miaka 50. Ambapo mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo alikuwa Mh. Majaliwa Kassimu Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye aliwakilishwa na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuuu- Uwekezaji Mhe. Angela Jasmine Kairuki.

 Pamoja na Maadhimisho hayo, TPDC ilitoa TUZO kwa baadhi ya WASTAAFU waliokuwa na michango mbalimbali katika utumishi wao. Pichani juu Bi Marie Msellemu, MKUU wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa TPDC, akimkabidhi Prof. Mark Mwandosya TUZO ya kuutambua mchango wake mkubwa kwa TPDC kwa nafasi yake kama Kamishna wa kwanza wa Petroli nchini na Mwenyekiti wa BODI ya Shirika la TPDC katika utumishi wake.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad